Donnarumma Apiga Goti Mbele ya Mwamuzi na Kuwa Kipa Mwenye Kadi Nyingi Zaidi za Njano Ulaya.

Gianluigi Donnarumma alionekana akiwa na hamu kubwa kuona bao la pili la Everton likifutwa siku ya Jumatatu, kiasi cha hata kupiga goti mbele ya mwamuzi Michael Oliver, kitendo kilichomletea kadi yake ya njano ya saba msimu huu, ikiwa ni nyingi zaidi kuliko kipa yeyote barani Ulaya.

Donnarumma Apiga Goti Mbele ya Mwamuzi na Kuwa Kipa Mwenye Kadi Nyingi Zaidi za Njano Ulaya.

Nahodha wa Italia Gianluigi Donnarumma alipokea kadi yake ya saba ya njano msimu huu siku ya Jumatatu, wakati wa sare ya 3-3 ya Manchester City dhidi ya Everton.

Kama ilivyoripotiwa na Goal.com, Gianluigi amepokea kadi nyingi za njano kuliko kipa yeyote katika ligi kumi bora barani Ulaya.

Donnarumma aliamini kuwa alifanyiwa madhambi katika ujenzi wa shambulizi lililozaa bao la pili la Everton, ambalo lilitokana na mpira wa kona. Hata hivyo, malalamiko yake kwa mwamuzi hayakuleta matokeo aliyoyatarajia.

Donnarumma Apiga Goti Mbele ya Mwamuzi na Kuwa Kipa Mwenye Kadi Nyingi Zaidi za Njano Ulaya.

Gianluigi Donnarumma, kipa wa Italia, alikuwa tayari amefanya michomo miwili muhimu ya kuokoa mabao kabla ya mechi, na kwa namna fulani alichangia katika bao la kusawazisha la dakika za mwisho la Manchester City baada ya kwenda juu ndani ya eneo la Everton kwenye mpira wa kona wa mwisho, ambao ulipelekea bao la Jérémy Doku.

Gianluigi yupo katika msimu wake wa kwanza na Manchester City, ambapo amefungwa mabao 40 katika mechi 40 katika mashindano yote, huku akiweka clean sheet 16.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.