Dylan Kerr Achukua Mikoba ya Aussems

Dylan Kerr aliyewahi kuinoa Klabu ya Simba ambao ni mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Bara amepewa kibarua cha kuinoa timu ya Black Leopards ya Afrika Kusini.

Kerr mwenye miaka 53 ana uzoefu na soka la Afrika kwa kuwa aliwahi kuinoa Klabu ya Baroka FC msimu wa 2020 ambapo aliibuka ndani ya klabu hiyo akitokea Klabu ya Black Leopards.

Pia aliwahi kuifundisha Klabu ya Gor Mahia msimu wa 2017/18 nchini Kenya baada ya kuchimbishwa ndani ya Simba aliyoifundisha msimu wa 2015/16.

Black Leopards imemrejesha tena Kerr ndani ya kikosi hicho baada ya kumfuta kazi Patrick Aussems raia wa Ubelgiji ambaye naye aliifundisha Simba kwa msimu wa 2019/20 na aliweza kutwaa taji la Ligi Kuu Bara.

Akiwa ndani ya timu hiyo alikiongoza kikosi hicho kwenye mechi tatu na zote alipoteza jambo ambalo limewafanya mabosi wa timu hiyo kumfuta kazi jumlajumla.

Habari kutoka Afrika Kusini zimeeleza :”Kerr atafanya kazi na Morgan Shivambu na Mongezi Bobe akichukua mikoba ya Aussems,” ilieleza taarifa hiyo.

Ndani ya Baroka FC, kocha huyo alifutwa kazi hivyo anarejea kwenye timu yake ya zamani akiwa huru.


BASHIRI UKIWA MAHALI POPOTE!

Hauhitaji kuwaza linapokuja suala la ubashiri na odds kubwa. Bashiri na Meridianbet ukiwa popote ufurahie ushindi mkubwa katika michezo mbalimbali na hadi milioni 16 kwenye michezo ya kasino.

Meridianbet Beti Popote

INGIA MCHEZONI!

 

20 Komentara

    pongezi kubwa sana kwake akapige kazi sasa

    Jibu

    Kapige kazi ss ujue umepewa dhaman kubwa!

    Jibu

    Kuna haja kubwa kukuza Makocha wazawa kuliko hawa wanazunguka kila Klabu na kufanya kazi muda mfupi na kufukuzwa kisha kuajiriwa tena Klabu nyingine

    Jibu

    Wazawa kwanza ingawa frusa hizi hazipatikani kwa wepisi wanapata wageni na mwishowe wakiharibu tu wanaondolewa

    Jibu

    Piga kazi kijana

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    Mtu wa kaz

    Jibu

    Dylan kerr mda wake sasa wa kufukia makosa yake

    Jibu

    Kazi kaz piga kaz

    Jibu

    Kazi nzuri kijana piga kazi

    Jibu

    Gundu linaendelea kwa Aussems

    Jibu

    piga kazi

    Jibu

    Maskini uchebe sijui anakwama wapi nako kafukuzwa

    Jibu

    Hongera

    Jibu

    Kijana Yuko vizuri apige kazi

    Jibu

    Piga kazi

    Jibu

    Jambo zur hili

    Jibu

    Jmaa yupo vizuri

    Jibu

    Uchebe zimu la msimbazi bado linamtafuna

    Jibu

    hongera yake

    Jibu

Acha ujumbe