Promota nguli wa masumbwi, Eddie Hearn amemtambua Logan Paul kama mshindi katika pambano la kujifurahisha dhidi ya Floyd Mayweather liliopigwa wikiendi iliyopita.
Logan aliweza kummudu Mayweather katika pambano la raundi nane, ambalo aliweza kumaliza raundi zote na bingwa huyo wa masumbwi na kuisha sare.
Floyd Mayweather mshindi mara tano wa dunia wa uzito wa juu alikiri kushangazwa na uwezo wa masumbwi wa Logan Paul ambaye ni staa wa youtube.
Lakini Eddie Hearn anaamini Mayweather hatakuwa na furaha baaada ya pambano hilo lililomrudisha ulingoni baada ya kustaafu masumbwi.
“Hakukuwa na maamuzi, ilikuwa ya kustaajabisha,” Hearn aliiambia Sky Sports
“Lakini ndio kama kuna mshindi katika pambano hilo basi ni Logan Paul, kwasababu nadhani ilikuwa mbaya kutoka kwa Floyd Mayweather.”
Chukua namba yako ya akaunti na kiasi cha pesa unachotaka kuweka, sogea kwenye duka lolote la Meridianbet lililo karibu nawe utasaidiwa kuweka pesa.
Alifanya kazi nzuri