Ederson Kutimka Man City

Golikipa namba moja wa klabu ya Manchester City raia wa kimataifa wa Brazil Ederson Moraes ana hatihati ya kutimka ndani ya klabu hiyo mabingwa wa Uingereza.

Ederson inaelezwa yupo kwenye kwenye mazungumzo na vilabu kadhaa kutoka nchini Saudia Arabia ambapo inaelezwa wamempa ofa kubwa golikipa huyo, Hivo inaelezwa kua nyanda huyo amevutiwa na ofa hizo na inawezekana kwa kiwango kikubwa atatimka klabuni hapo.edersonKocha wa Manchester City Pep Guardiola ameweka wazi bado hajajua kama golikipa huyo ataendelea kusalia ndani ya klabu kuelekea msimu ujao, Kauli ya Guardiola imeonesha wazi kua kuna asilimia kubwa kwa golikipa huyo kutimka ndani ya timu hiyo kuelekea msimu ujao.

 

Klabu ya Al-Ittihad inaelezwa imeshakubaliana maslahi binafsi na Ederson na kilichobaki ni klabu hiyo inayoshiriki ligi kuu ya Saudia Arabia kutoa kiasi cha pesa ambacho klabu ya Man City wanakihitaji, Baada ya kumalizana na Man City ni wazi kua golikipa huyo raia wa kimatiafa wa Brazil anaweza kutimka klabuni hapo.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.