Mchezaji kinda wa Manchester United, Facundo Pellistri, anaweza kutolewa kwa mkopo klabuni hapo katika dirisha hili la usajili.
Haya yanajiri baada ya wakala wa Facundo Pellistri – Edgardo Lasalvia kuthibitisha Hispania inaweza kuwa ndio sehemu atakayokwenda mchezaji huyo.
Pellistri alisajiliwa na United mwezi Oktoba 2020 akitokea katika klabu ya Penarol inayocheza ligi kuu nchini Uruguay. Licha ya kuwepo kwenye orodha ya wachezaji wa ziada kwenye benchi la United katika mechi 2 za UEFA (PSG na Istanbul Basaksehir), Facundo bado hajacheza mchezo wowote wa EPL.
Mapema wiki hii, mtandao wa Manchester Evening News (MEN), uliripoti utayari wa United kumruhusu Facundo kwenda kucheza kwenye timu nyingine kwa mkopo, lengo likiwa ni kumjengea uzoefu wa kucheza soka la Ulaya.
“Tunalifanyia kazi. Ni kweli, (Facundo) anaweza kwenda Hispania.” Alisema Edgardo baada ya kuulizwa uwezekano wa Pellistri kuondoka United mwezi huu.
Pokea mualiko wa Meridianbet na Pragmatic Play kutengeneza mkwanja kwenye kasino ya mtandaoni sasa. Jiunge sasa kupata ishindi huu.
Adelta
Pole yake
Sania
Usajili umepamba moto
Rahmal
Pole sana facundo
Shakila mrope
Pole san kijana
Magdalena
Duh hii kali
Dorophina
Kambi popote facundo kikubwa masrahi tu
Sadick
Hii ndio changamoto ya vilabu vikubwa kusajiri wachezaji wengi wasiowahitaji sana mwisho wanaishia kucheza kwa mikopo sehema mbalimbali na anapofanya vzr kwenye club aliyopelekwa na club husika ikataka kumusajiri moja kwa moja tatizo huanzia hapo
Caroline
Poleni sana
Lydia Emmanuel Magoti
Duu pole yake
Hopemwaikuka
Dah
Sarah
Pole yake
Ernest Kimeru
Sio mbaya akajifunze kwingine huenda pia akapata muda mwingi wa kucheza
Issa
Wampe muda
Venerose
Mmmh
Angelina
Duuh
warda
Wamtoe tu sio mbaya