FIFA Kufungia Usajili Simba SC

Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) limeifungia klabu hiyo kusajili kwa kipindi kimoja kijacho cha usajili.

Hukumu hiyo ya FIFA imekuja kufuatia shirikisho hilo kuikuta na hatia Simba kutokana na kushindwa kumalizana na beki wao wa zamani, Mghana Asante Kwasi.

Taarifa kutoka nchini Ghana zinasema adhabu hiyo kwa Simba itaanza kufanya kazi katika dirisha lijalo la usajili.

FIFA

Imeelezwa kuwa Simba ilipewa muda wa kukamilisha malipo ya mchezaji wao wa zamani, Asante Kwasi ambaye alipeleka malalamiko yake Shirikisho la Soka Duniani, (FIFA) ili kupata stahiki zake.

Kwa mujibu wa barua ambayo waliandikiwa Simba kutoka Shirikisho la Soka la  mpira la Ghana, PFAG liliwaeleza kuwa wanapaswa kumlipa mchezaji huyo stahiki zake baada ya kushinda rufaa.

Barua hiyo iliandikwa Februari 26,2021 zama za Mtendaji Mkuu, Senzo Mbatha ambaye kwa sasa ni Mshauri wa kuelekea kwenye Mabadiliko ndani ya Yanga.

FIFA

Maamuzi ya Fifa yalifanyika awali Januari 15,2020 na pia shauri la pili likatolewa maamuzi Februri 2021 baada ya mchezaji huyo kukata rufaa.

FIFA iliwaambia Simba kwamba wanapaswa kulipa kiasi cha USD 4,000 kwa ajili ya malipo ya stahiki za mchezaji Kwasi ambaye alicheza Simba akitokea Klabu ya Lipuli.

Habari zimeeleza kuwa Simba wamepewa muda kukamilisha malipo ya mchezaji huyo ambaye msimu wa 2017 alicheza Lipuli akitokea Klabu ya Mbao na aliachwa Simba msimu wa 2019


MKWANJA MARIDHAWA NA KASINO YA 777 MEGA DELUXE

Nafasi nyingine kwaajili yako, kasino mpya yenye hadhi ya kipekee inayokupa kila sababu ya kuwa mshindi katika kasino za Meridianbet, anza siku yako na njia rahisi ya kutengeneza mkwanja.

CHEZA HAPA

9 Komentara

    Kweli penye riziki hapakosi fitina Simba inaelekea kwenye mafanikio ndo kesi kila siku zinaibuka ila watashinda tu

    Jibu

    Ee jamani pole yao klabu ya simba ila yatakwisha na ushindi lazima#meridianbett#

    Jibu

    Wanafanya vibaya

    Jibu

    Sawa tu ila simba iko kwenye mafanikio

    Jibu

    Duuh sio powa kabisa

    Jibu

    Wanahisi wanakomoa kumbe ndo kwanza wanazidi kuwafungulia milango ya baraka

    Jibu

    Majungu hayo

    Jibu

    Sio poa

    Jibu

    Duuh sio poa

    Jibu

Acha ujumbe