Fiorentina bado wanamuwinda mlinda mlango na wamepania kumnunua kipa wa Chelsea, Kepa Arrizabalaga.

Viola wako katika hatua za awali za mradi mpya chini ya kocha Raffaele Palladino na tayari wamekuwa wakifanya kazi sokoni, wakikamilisha mikataba ya Marin Pongracic, Moise Kean na Andrea Colpani. Sasa wanasukumana kumchukua Albert Gudmundsson wa Genoa na Tanner Tessmann wa Venezia.
Pia meridianbet inatoa michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.

Fiorentina pia wamekuwa wakitafuta mlinda mlango mpya atakayeanza kuchukua mikoba ya Pietro Terracciano na walikuwa wakihusishwa kwa ufupi kutaka kumnunua mkongwe wa zamani wa Manchester United David de Gea. Mkataba haujakamilika kwa Mhispania huyo kwa sababu ya madai yake ya juu ya mshahara.
Taarifa kutoka Uhispania la DefensaCentral linaeleza jinsi Fiorentina wanafikiria kwa dhati kumnunua Kepa Arrizabalaga katika wiki zijazo, wakifahamu kwamba anaweza kuondoka Chelsea kwa takriban €5m ikizingatiwa kwamba amebakiza chini ya mwaka mmoja kwenye mkataba wake.



