Rb Leipzig Wamtamani Xavi Simons Jumla

Klabu ya Rb Leipzig imemtamani kiungo wa kimataifa wa Uholanzi Xavi Simons kwa uhamisho jumla kutokana na ubora ambao anauonesha kinda huyo ambaye yupo kwa mkopo klabuni akitokea klabuni hapo.

Mkurugenzi wa klabu ya Rb Leipzig Eberl anasema wataangalia namna ya kuweza kumbakiza Xavi Simons klabuni hapo kwa muda mrefu zaidi baada ya mkataba wake wa mkopo kumalizika mwaka 2024.Rb LeipzigKiungo Xavi Simons amekua na kiwango bora sana ndani ya klabu hiyo inayoshiriki ligi kuu nchini Ujerumani, Huku akiwa amefanikiwa kuchangia mabao sita ndani ya klabu hiyo mpaka sasa akiwa amefunga matatu na kutoa pasi tatu za mabao.

Klabu ya Rb Leipzig wao wanaona kama wanaweza kuhakikisha wanaongeza muda wa kuendelea kummiliki mchezaji huyo kinda mwenye kipaji kikubwa raia wa kimataifa wa Uholanzi ambaye amewahi kukipiga timu ya vijana ya Barcelona.Rb LeipzigKlabu ya PSG wao kwa upande wao wanamtoa kwa mkopo mchezaji huyo ili kumpa ukomavu mkubwa, Kwani wana mipango mikubwa na mchezaji huyo siku za mbeleni kwakua wanaamini kwenye kipaji kikubwa alichonacho Xavi Simons.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.