Klabu ya Rb Leipzig inaelekea kushinda mpambano wa kumbakiza kiungo wa kimataifa wa Uholanzi Xavi Simons ndani ya klabu hiyo licha ya ushindani mkubwa waliokutana nao.
Rb Leipzig wanamuhitaji Xavi Simons aendelee kuwatumikia kwa mkopo kama ambavyo aliwatumikia msimu uliomalizika, Kwani klabu yake ya PSG haipo tayari kumuuza hivo njia pekee ya kumpata kiungo huyo ni kuendelea kumtumia kwa njia ya mkopo kuelekea msimu ujao.Klabu hiyo imekutana na upinzani mkali sana katika kumuwania kiungo huyo kwani klabu ya Bayern Munich imekua ikipambana kwa kiasi kikubwa kumpata kiungo huyo, Lakini kiungo Xavi Simons inaelezwa ameonesha taa ya kijani kwa klabu ya Leipzig kua yupo tayari kuwatumikia.
Klabu ya Manchester United inaelezwa pia ilikua inafukuzia saini ya Xavi Simons huku wao wakielezwa walikua wanahitaji kumnunua kabisa na sio kumchukua kwa mkopo, Lakini mpaka sasa Rb Leipzig ndio wanaonekana kukaribia kushinda mpambano huu mkali uliohusisha vilabu vitatu.
This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.
Strictly Necessary Cookies
Strictly Necessary Cookie should be enabled at all times so that we can save your preferences for cookie settings.
If you disable this cookie, we will not be able to save your preferences. This means that every time you visit this website you will need to enable or disable cookies again.