Mike Arteta amelaumiwa kwa kichapo cha 3-1 cha Arsenal dhidi ya West Ham na kuwafanya waondoshwe kwenye Kombe la Carabao.
kocha wa Gunners Arteta alifanya mabadiliko sita katika Uwanja wa London Stadium na timu yake ilichapwa vikali kutokana na bao la kujifunga la Ben White na mabao ya Mohammed Kudus na Jarrod Bowen.
Moja ya mabadiliko makubwa aliyoyafanya Mhispania huyo ni kumchagua Declan Rice kwenye benchi aliporejea The Hammers kwa mara ya kwanza tangu alipohamia London Kaskazini kwa pauni milioni 100 majira ya joto.
Baada ya kukosa nafasi ya robo fainali, Arteta alisema: “Nimesikitishwa sana. Ninawajibika kwa hilo, tumetoka kwenye kombe, tulitaka kucheza mchezo tofauti sana na kushindana. Mchezo ulichukua mwelekeo kwa sababu ya bao la kwanza lakini lazima tuone mengi zaidi kutoka kwa timu na kupata haki ya kushinda.”
Kocha huyo anasema kuwa amesikitishwa na nafsi yake. Walitaka kucheza kwa njia tofauti na hawakuweza kufanya hivyo. Kila wanapopoteza maumivu yapo. Wanapaswa kutumia maumivu haya na kushindwa huku kuandaa njia bora kwa Newcastle siku ya Jumamosi.
Meneja David Moyes alisema, ilikuwa utendaji mzuri wa timu. Wachezaji wa mbele walifanya kazi nzuri sana na kwa muda mrefu walikuwa wazuri katika ulinzi. Kwa sehemu kubwa walipambana vyema.
Labda wanakuwa timu nzuri ya kikombe. Anataka kuwa timu nzuri ya ligi ikiwa anaweza kuwa lakini ikiwa hawezi kabisa kufanya hivyo basi lazima wafanye vizuri kwenye vikombe ikiwa wanaweza.
“Tumeshinda tu dhidi ya Arsenal, hatupati mataji kwa hilo.”
Wapinzani wa Arsenal siku ya Jumamosi Newcastle wanakuja kwenye mpambano wa Ligi Kuu ya Uingereza wakiwa juu baada ya kuwalaza Manchester United 3-0 katika uwanja wa Old Trafford.