Chelsea imehusishwa katika uhamisho wa golikipa wa Bayern Munich, Manuel Neuer, lakini Mjerumani hiyo hatamani kuhamia Stamford Bridge, kwasababu hataki kucheza nje na anahitaji kushinda mataji meingi zaidi akiwa na klabu ya sasa. Neuer mwenye miaka 34 mkataba wake na Bayern unamalizika mwaka 2021 msimu wa majira ya joto, na makubaliano kuhusu mkataba mpya hayajafanyika hivyo kufanya mstakabali wake kutokueleweka.
Alexander Nubel amesajiliwa bure kutoka Schalke na ana miaka the 23 inaonekana ni mbadala wa muda mrefu wa Neuer, anahitaji mkataba mpya kabla ya awali haijamalizika, lakini inaoekana anawezekana hilo lisitimie. Amekuwa moja ya magolikipa bora kutokea duniani. Kwasasa Bayern kama hawahitaji huduma yake tena.
Neuer hana mpango wakucheza nje ya Ujerumani, katika maisha yake ya soka amecheza akiwa nyumbani. Chelsea wameonyesha nia ya kumsajili mkongwe huyo japo, hana mpango wakuhamia Uingereza.
Neuer bado anaamini atashinda Klabu Bingwa kwa mara ya pili akiwa na Bayern na anafahamu hilo linaweza kuwa gumu akiwa nje ya Bavaria. Hata kama mkataba wa Neuer hautaongezwa bado atabaki chaguo la kwanza Bayern hawatakubali kumuachia.
Chelsea inahitaji kupata golikipa mpya chini ya kocha Frank Lampard kwani bado hajashawishika na kiwango cha Kepa Arrizabalaga na mkongwe Willy Caballero.
Kipa wa AC Milan, Gianluigi Donnarumma na Burnley, Nick Pope pia wamehusishwa kutua Stamford Bridge.
Issa
Chelsea inabidi wakaze kumtwaa pale bayern wanatakiwa waweke mpunga