Chelsea wamethibitisha kuwa Edouard Mendy amefanyiwa upasuaji baada ya kuumia akiwa mazoezini. Odds kubwa za soka unazipata meridianbet, Bashiri kibingwa.
Kipa huyo hajaichezea CHELSEA tangu Kombe la Dunia, na amekabiliwa na vita ya kuingia kwenye kikosi tangu Graham Potter alipowasili. Kepa Arrizabalaga amekuwa akiaminiwa kwa kiasi kikubwa na kocha wa Chelsea.
Mendy hakuweza kuhusika dhidi ya Manchester City katikati ya wiki, mchezo ambao Kepa alikabiliwa na maswali kuhusu jukumu lake katika ushindi wa Riyad Mahrez. Unaweza kubashiri Mubashara na Meridianbet Bonyeza hapa ambapo kabla ya mechi hiyo, Potter alikuwa na furaha katika tathmini yake ya hali ya jeraha la Mendy.
“Amekuwa akifanya mazoezi zaidi ya alivyokuwa,” Chelsea ilisema katika mkutano wake na waandishi wa habari kabla ya mechi.
“Hayuko sawa kabisa kwa sasa lakini tunatumai katika wiki ijayo au hivyo anaweza kufanya maendeleo.”
Hata hivyo, Mendy amevunjika kidole akiwa mazoezini na sasa amefanyiwa upasuaji huo, ikimaanisha kuwa anakabiliwa na tatizo jingine nje ya uwanja. Tembelea duka la kubashiri uoneshe umwamba wa kubashiri.
Inaongeza orodha kubwa ya majeruhi inayomkabili Potter, huku wachezaji kumi wa kikosi cha kwanza cha Chelsea wakiwa hawapatikani kwa sasa.
Huku Reece James, N’Golo Kante, Wesley Fofana na Ben Chilwell wakiwa tayari ni miongoni mwa wale waliokuwa nje, Mason Mount alipata jeraha katika mazoezi na kumfanya akose mechi ya City, kabla ya Raheem Sterling na Christian Pulisic kulazimishwa kutolewa nje ndani ya dakika 20.
“Sijawahi kupata kitu kama hicho na nisingependa kuiona hapa,” Potter alisema.