Raisi wa klabu ya Barcelona Joan Laporta ameelezea uvamizi uliofanywa na mashabiki karibia 30,000 ambao walivamia uwanja huo licha ya klabu hiyo kupatiwa tiketi 5,000 kwa ajiri ya mashabiki wao.
Beki wa kati Ronald Araujo na kocha wa klabu hiyo Xavi Hernández licha ya wote kwa pamoja kulizungumzia swala hilo baada ya mchezo kuisha, wote walisema kushangazwa na uvamizi uliofanywa na mashabiki hao ambapo ilikwenda kuwa mada kwenye vyumba vya kubadilishia nguo.

Raisi wa klabu hiyo Joan Laporta pia alielezea swala hilo kwenye Barca TV baada ya mchezo, na kuahidi kuna uchunguzi na hatua kuchukuliwa ili kuzuia swala hilo lisijitokeze tena.
“Ni aibu ambayo tumeipata leo, haiwezi kutokea tena, Tunataarifa nyingi kuhusu kilichotokea na tunahitaji muda kupitia. Kisha tutachukua hatua, tutawaelezea na haitatikea tena kwa sababu tunathubitisha.
“Hatuwezi kuepuka swala hili lakini kwa sasa tutakuwa waangalifu na kuangailia nini tusikuruhusu kutokea kwa hapo baadae. Tumepitia mambo ambayo hatuhitaji. Kama mwana Barcelona naona aibu na kiukweli niwaombe msamaa kwa kilichotokea.” Alisema — Joan Laporta
Tiketi 25000 za mashabiki wa Eintract Frankfurt walinunua kutoka kwa mashabikiwa klabu ya Barcelona ambao hawakutaka kwenda uwanjani.
Maana halisi ya ushindi mkubwa unaipata katika kasino ya mtandaoni ya Aviator kutoka meridianbettz. Andaa kapu la ushindi wa mkwanja na beti kibao za BUREEE.