PSG wameshinda ubingwa wa rekodi wa 14 wa ligi ya Ufaransa siku ya Jumatano baada ya kuifunga Lens mabao 2-0, na hivyo kutwaa taji lao la tano mfululizo la Ligue 1.

Khvicha Kvaratskhelia alifungua ukurasa wa mabao kabla ya mchezaji wa akiba Ibrahim Mbaye kuongeza bao la pili na kuhakikisha PSG hawafikiwi na wapinzani wao wakiwa na mechi moja mkononi.
Kvaratskhelia alifunga bao lake la 19 la msimu baada ya Ousmane Dembélé kumtengenezea bao la kwanza, huku Mbaye akifunga bao la dakika za nyongeza.
Ushindi huo unawapa PSG ubingwa wa 14 wa Ligue 1, ambapo 12 kati ya hizo zimepatikana ndani ya miaka 14 chini ya umiliki wa Qatar. Klabu hiyo ilikuwa tayari imekaribia kutwaa ubingwa huo wikiendi iliyopita baada ya kushinda dhidi ya Stade Brestois.



