Hatimaye uongozi wa PSG umethibitisha kukatisha mkataba na aliyekuwa kocha wa timu hiyo – Thomas Tuchel.
Tuchel alisimamishwa kazi siku ya mkesha wa Krismasi ikiwa ni miezi 4 tu tangu aiongoze timu hiyo kwenye fainali ya Ligi ya Mabingwa.
Hapakuwa na taarifa rasmi kutoka PSG kuhusu tukio hilo ambalo linahusishwa na Mauricio Pochettino kujiunga na miamba hiyo ya soka la Ufaransa – Ligue 1.
Leo, raisi wa PSG – Nasser Al-Khelaifi amethibitisha hilo. Nasser amesema “Nina mshukuru Thomas Tuchel na benchi lake la ufundi kwa aliyoyafanikisha kwenye klabu yetu.

“Thomas aliweka nguvu kubwa kwenye kazi yake na tutamkumbuka kwa nyakati zote tulizokuwa pamoja. Tunamtakia kila la kheri katika kazi yake.”
Taarifa ya kuthibitisho zimechelewa kutokana na taratibu za kisheria hasa fidia ambayo Tuchel anapaswa kulipwa, kocha huyo atapokea takribani pauni milioni 5 kama sehemu ya fidia yake.
Huwenda Pochettino atatangazwa kama kocha mpya wa klabu hiyo baada ya kuwa nje ya benchi la ufundi tangu Septemba 2019.
VUNA SHEA YAKO YA 230,000,000TSH NA UFURAHIE MSIMU HUU WA SIKUKUU!!!
Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, jiwekee nafasi ya kupata shea yako ya 230,000,000Tsh kupitia mchezo wa Secret Santa. Hakika hutojutia kufurahia msimu huu wa sikukuu ukiwa katika nyumba ya mabingwa ya Meridiabet. Unasubiri nini?




Angelina
Kila la kheri
Ernest Kimeru
Huenda tukamuona Tuchel Uingereza ndani ya EPL
Hopemwaikuka
Pole Tuchel
Issa
Mmh psg inasua msimu huu
Rahmal
Tuchel pole
Shakila mrope
Mhh ata sijui cha kuandika
Neema juma
Kila la kheri
Dorophina
Kweli vilabu vingi vya soka havitaki masihara ukizingua wanakutema
Saupha mohamed
Kwaheri kocha
Lydia Emmanuel Magoti
Pole yake
Fatina mfingi
Pole utaenda kokote Kule
Mwanahamisi
Pole yake
warda
Nilikuwa namkubali sana Tuchel
Tatu
Popote kambi
Sarah
Pole yake
Zahara omary
Pole yake
Sania
Kambi popote
Chiku
Kocha usikate Tamaa maisha popote