Klabu ya PSG ipo mbioni kumalizana na aliyekua kocha wa klabu ya Barcelona na timu ya taifa ya Hispania Luis Enrique kama kocha wao mkuu kwa msimu ujao.
Klabu ya PSG imefikia hatua nzuri katika mazungumzo baina yao na kocha Enrique ili kuweza kumsaini kocha huyo aiongoze timu hiyo kuanzia msimu ujao baada ya kocha wa zamani wa Bayern Munich Julian Nagelsman kuikataa timu hiyo.
Mabingwa hao wa Ufaransa wanahaha kupata kocha mwenye ubora sokoni kwasasa kwani tayari wameshafanya mazungumzo na makocha kadhaa mpaka sasa kabla ya Enrique, Lakini bado hawajafanikiwa kumpata kocha mkuu wa timu hiyo msimu ujao.
Klabu ya PSG imekua ina uchu mkubwa wa kutwaa taji la ligi ya mabingwa ulaya kutokana na uwekezaji ambao wamekua wakiufanya ndani ya klabu hiyo, Huku makocha wengi wakiondolewa hapo kutokana na kushndwa kufikia malengo hayo.
PSG imekua ikifukuza makocha mara kwa mara kwasababu ya kushindwa kutwaa taji la ligi ya mabingwa, Lakini Enrique kama atafanikiwa kupewa timu hiyo anaweza kuwafikisha nchi ya ahadi kwani kocha huyo ana uzoefu wa michuano hiyo kwani tayari ameshawahi kutwaa taji hilo na Barcelona.

