Mshambuliaji wa klabu ya FC Nantes, Mostafa Mohamed ameondolewa katika kikosi cha awali cha timu ya taifa ya Egypt kitakachojiandaa kwa Kombe la Dunia 2026, hatua iliyoshangaza wengi kutokana na uzoefu wake.
Katika kikosi hicho, kocha Hossam Hassan amemjumuisha mchezaji kijana asiye na uzoefu wa kimataifa, Hamza Abdelkarim, anayekipiga katika kikosi cha vijana cha FC Barcelona chini ya umri wa miaka 19, kutokana na kiwango chake bora.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Nahodha wa timu hiyo, Mohamed Salah wa Liverpool, ataongoza safu ya ushambuliaji akishirikiana na Omar Marmoush wa Manchester City katika mashindano yatakayofanyika Marekani, Canada na Mexico.
“Mostafa Mohamed ameondolewa kutokana na kiwango chake kushuka, huku akifunga mabao manne pekee katika mechi 24 msimu huu,” ilieleza taarifa ya timu ya taifa ya Misri.
“Badala yake, tumempa nafasi kijana Hamza Abdelkarim kutokana na maendeleo makubwa aliyoyonyesha katika kikosi cha vijana cha Barcelona,” alisema kocha Hossam Hassan.
Misri itacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Russia mjini Cairo Mei 28 kabla ya kuelekea Marekani kwa maandalizi ya mwisho ya Kombe la Dunia.
“Tuna timu yenye mchanganyiko wa uzoefu na vipaji vipya, na lengo letu ni kufanya vizuri katika Kombe la Dunia,” aliongeza Hassan.
Katika michuano hiyo, Misri ipo Kundi G ambapo itakutana na Brazil, Belgium na New Zealand katika hatua ya makundi.


