Refa Omar Artan Apokelewa Kifalme Nchini Somalia

Mwamuzi wa mpira wa miguu kutoka Somalia, Omar Artan, amerejea nyumbani mjini Mogadishu na kupokelewa kwa heshima kubwa kama shujaa licha ya kushindwa kutimiza ndoto yake ya kuchezesha Kombe la Dunia la FIFA 2026 baada ya kunyimwa ruhusa ya kuingia nchini Marekani.

Refa Omar Artan Apokelewa Kifalme Nchini Somalia Artan, mwenye umri wa miaka 34, alikuwa amechaguliwa na FIFA kuwa miongoni mwa waamuzi watakaosimamia mechi za mashindano hayo makubwa duniani. “Ilikuwa fursa ya kipekee si kwangu tu bali kwa taifa zima la Somalia,” alinukuliwa akieleza baada ya kurejea nchini kwake.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa, mwamuzi huyo alizuiwa na mamlaka za uhamiaji alipowasili katika mji wa Miami, licha ya kuwa na pasipoti ya kidiplomasia pamoja na visa halali ya Marekani. “Nilifuata taratibu zote zinazohitajika, lakini sikuruhusiwa kuingia nchini,” alisema Artan.

Refa Omar Artan Apokelewa Kifalme Nchini Somalia Tukio hilo limezua hisia kali miongoni mwa wadau wa soka nchini Somalia na Afrika kwa ujumla, huku wengi wakieleza masikitiko yao kutokana na kupotea kwa nafasi ya kihistoria ambayo ingemfanya kuwa mwamuzi wa kwanza kutoka Somalia kuchezesha Kombe la Dunia.

Refa Omar Artan Apokelewa Kifalme Nchini Somalia Licha ya changamoto hiyo, mamia ya wananchi walijitokeza kumpokea alipowasili Mogadishu, wakimtambua kama mfano wa mafanikio na uthubutu. “Kwetu bado ni shujaa, kwa sababu amefika mahali ambapo WaSomalia wengi hawajawahi kufika katika soka la kimataifa,” alisema mmoja wa mashabiki waliojitokeza kumpokea.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.