Klabu ya AS Roma imethibitisha kufanya usajili wa kudumu wa mshambuliaji wa Uholanzi Donyell Malen baada ya klabu hiyo kufanikisha lengo la kufuzu kushiriki Ligi ya Europa msimu ujao.
Malen alijiunga na Roma kwa mkopo akitokea Aston Villa FC katika dirisha la usajili la Januari, akiwa na kipengele cha uhamisho wa lazima wa €25 milioni kilichokuwa kimefungwa katika makubaliano yao.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Kipengele hicho kilitekelezwa baada ya Roma kufanikiwa kumaliza katika nafasi ya kufuzu michuano ya Ulaya, iwe Ligi ya Mabingwa au Ligi ya Europa, na hivyo kuifanya dili hiyo kuwa ya kudumu rasmi.
Kwa sasa Roma wapo nafasi ya tano wakiwa na pointi 67, sawa na AC Milan walio katika nafasi ya nne, huku Como 1907 wakiwa nyuma kwa pointi mbili, ligi ikiwa imebakiwa na mechi mbili pekee kumalizika.
Tangu ajiunge na Olimpico, Malen ameonyesha kiwango cha juu akifunga mabao 13 na kutoa pasi mbili za mabao katika mechi 16 za Serie A, na kujijengea nafasi muhimu katika kikosi cha Roma.
Akizungumza kuhusu usajili huo, msemaji wa klabu alisema “Malen ameonyesha ubora mkubwa tangu alipojiunga nasi. Tumefurahishwa sana na mchango wake na anaendelea kuwa sehemu muhimu ya mipango yetu ya baadaye.”


