Bennacer Ajifunga Milan Mpaka 2027

Kiungo wa klabu ya Ac Milan Ismael Bennacer raia wa kimataifa wa Algeria amesaini kandarasi mpya ya kuendelea kuitumikia klabu ya Ac Milan Mpaka mwaka 2027.

Kiungo Bennacer alikua anafanya mazungumzo n klabu ya Ac Milan kwa wiki kadhaa nyuma ili koungeza mkataba na mabingwa hao watetezi wa ligi kuu ya Italia Serie A. Mazungumzo baina ya mchezaji huyo na klabu ya Ac Milan yamemalizika na mchezaji huyo ataendelea kusalia klabuni hapo kwa muda mrefu.bennacerIsmael Bennacer amekua mchezaji muhimu kwenye kikosi cha Ac Milan chini ya kocha Stefano Pioli, Hivo klabu hiyo ikaona umuhimu wa kiungo huyo na kuamua kumuongezea mkataba aendelee kusalia ndani ya klabu hiyo.

Kocha wa klabu ya Ac Milan ni mtu ambae amehakikisha kua mchezaji huyo anasalia ndani ya viunga vya Milan, Kwani kocha Pioli ndio alipendekeza kiungo huyo aongezewe mkataba kwani ni miongoni mwa wachezaji ambao ni muhimu kwenye mipango yake.bennacerKiungo Ismael Bennacer amesaini mkataba wa kuitumikia klabu ya Ac Milan ambao utamueka klabuni hapo mpaka mwaka 2027, Lakini kwenye kipengele cha mkataba wake mchezaji huyo ataruhusiwa kuuzwa kama klabu yeyote itafika kiasi cha Euro milioni 50 ambayo ndio itakua thamani ya kuvunja mkataba wa kiungo huyo ndani ya Milan.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.