Donyell Malen Amesaini Mkataba na AS Roma Utakaomuweka Klabuni Hapo Hadi Mwaka 2030.

Donyell Malen amefichua nafasi kubwa aliyocheza Gian Piero Gasperini katika kumshawishi kujiunga na AS Roma, huku mshambuliaji huyo wa Uholanzi akizungumza kwa mara ya kwanza tangu kusaini mkataba wa kudumu na Giallorossi hadi mwaka 2030 baada ya kuwa na msimu wa kwanza wa kuvutia sana katika jiji la Rome.

Donyell Malen Amesaini Mkataba na AS Roma Utakaomuweka Klabuni Hapo Hadi Mwaka 2030.
 

Mchezaji huyo mwenye miaka 27, aliyefunga mabao 14 katika mechi 18 za Serie A na kusaidia Roma kufuzu kucheza UEFA Champions League, alimiminia sifa nyingi kocha aliyefungua uwezo wake baada ya kipindi kigumu akiwa Aston Villa.

“Nini kilinishawishi? Bila shaka jina la Roma na klabu yenyewe, lakini pia malengo ya klabu na kocha wetu,” alisema Malen kupitia Retesport.it. “Tulipozungumza, kwa maneno machache tu alinifanya nijisikie muhimu mara moja na sehemu kuu ya mradi huu.”

Alipoulizwa kama alitarajia kuwa na athari kubwa na ya haraka kiasi hicho katika Serie A, Donyell Malen alionyesha unyenyekevu katika majibu yake.

“Kwa hakika nilitumaini na kutarajia kufanya vizuri. Lakini kama nimefikia kiwango hiki na kufunga mabao mengi namna hii, nawadaiwa zaidi wenzangu wa uwanjani pamoja na kocha ambaye tangu mwanzo aliniweka katikati ya safu ya ushambuliaji.”Alisema

Donyell Malen Amesaini Mkataba na AS Roma Utakaomuweka Klabuni Hapo Hadi Mwaka 2030.

Akizungumzia bao lake muhimu zaidi akiwa na jezi ya AS Roma, Donyell Malen hakuchagua lile la kuvutia zaidi, bali lile lenye maana kubwa zaidi.

“Huenda si bao zuri zaidi kwa sababu lilikuwa penalti, lakini penalti niliyofunga dhidi ya Parma ilikuwa muhimu sana kwa nafasi yetu kwenye ligi,” alisema. “Katika wakati huo pia nilihisi kwa nguvu sana furaha ya mashabiki wetu.”

Malen pia alizungumzia kulinganishwa kwake na mshambuliaji nguli wa Brazil Ronaldo Nazário, jambo ambalo limekuwa likizungumzwa na mashabiki wa Roma.

“Ronaldo alikuwa mchezaji wa kiwango tofauti kabisa. Lakini kwangu inatosha kufunga mabao na kuyafunga kwa ajili ya Roma, huku nikiisaidia klabu kufikia malengo yake.” Alisema

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.