La Gazzetta dello Sport inaripoti Rafael Leao atafanyiwa uchunguzi wa kimatibabu kati ya leo na kesho lakini hakuna uwezekano kumuona mshambuliaji huyo wa Ureno akianza dhidi ya Atalanta Jumamosi.
Leao alikosa mechi tatu za mwisho za mashindano yote kutokana na jeraha la paja na Stefano Pioli alisema wiki iliyopita kwamba Rossoneri wangefanya ‘chochote’ ili aweze kupatikana dhidi ya Atalanta katika mechi inayofuata ya Serie A Jumamosi, Desemba 9.
Meridianbet inakukumbusha kubeti na Meridianbet kwa odds kubwa na machaguo kibao, pia unaweza kubashiri mubashara mechi zote.
Kulingana na La Gazzetta dello Sport, Rafael atafanyiwa uchunguzi wa kimatibabu leo au kesho. Ikiwa paja la Leao limepona, madaktari wa Milan wataanza awamu ya pili kumruhusu Leao kufanya kazi uwanjani na kuongeza mzigo wa kazi kwa wiki.
Hata hivyo, Gazzetta linadai kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 ana nafasi ndogo ya kuanza dhidi ya Atalanta Jumamosi, lakini anaweza kushiriki katika kikosi cha kwanza cha Rossoneri siku nne baadaye wakati vijana wa Pioli watakaposafiri kwenda Newcastle kwa mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa ambao Milan lazima ishinde kuweka matumaini yao ya kufuzu.