Mshambuliaji wa Napoli, Romelu Lukaku, anatarajiwa kurejea kikosini rasmi, hatua inayotajwa kuongeza matumaini kwa timu ya taifa ya Ubelgiji kuelekea mashindano ya FIFA World Cup mwezi ujao.
Kwa mujibu wa ripoti za vyombo vya habari vya Italia, Lukaku amerejea Napoli baada ya kukaa kwa wiki tano nchini Ubelgiji akipatiwa matibabu ya majeraha ya muda mrefu. Hata hivyo, mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 32 alitozwa faini na klabu hiyo baada ya kushindwa kurejea mara baada ya mapumziko ya mechi za kimataifa mwezi Machi.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Inaelezwa kuwa Lukaku alichagua kubaki Ubelgiji ili kuendelea na matibabu chini ya mtaalamu wake binafsi wa viungo, jambo lililosababisha Napoli kumkata asilimia 20 ya mshahara wake wa mwezi. Baadaye alirejea klabuni Aprili 20, lakini akarudishiwa ruhusa ya kuendelea na matibabu nje ya Italia.
Kocha wa Napoli, Antonio Conte, alionesha kutoridhishwa na mwenendo wa mchezaji huyo akisema “Sikupata nafasi ya kuzungumza naye. Najua mmoja wa viongozi wetu alizungumza naye, lakini hakukuwa na mawasiliano ya moja kwa moja kati yetu.”
Conte aliongeza kwa masikitiko “Alifika katika kituo cha mazoezi, lakini hakuna aliyegonga mlango wa ofisi yangu. Hilo liliniumiza, nilitegemea hata salamu au ujumbe wowote. Katika hali kama hizi, kocha hujaribu kuelewa kila mtu, lakini hakuna anayejitahidi kumuelewa kocha.”
Licha ya changamoto hizo, kurejea kwa Lukaku kunakuja wakati muhimu kwa Napoli ambao wako nafasi ya pili katika Serie A, huku wakiwa na michezo mitatu iliyosalia msimu huu. Kwa upande wa timu ya taifa ya Belgium, Lukaku tayari amefunga mabao 89 katika mechi 124, na anatarajiwa kuwa sehemu muhimu ya kikosi kitakachocheza dhidi ya Misri, Iran na New Zealand katika Kundi G la Kombe la Dunia.


