Marcus Thuram alikuwa amefunga bao la kwanza katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Parma, ushindi uliowezesha Inter Milan kutwaa Scudetto wakiwa na mechi tatu mkononi.
Mara tu baada ya mechi, Thuram aliposti picha kwenye Instagram ikimuonyesha akiwa na mataji mawili ya Scudetto aliyoyashinda wakati wa kipindi chake katika Stadio Giuseppe Meazza.

Ilikuwa ni picha iliyohaririwa, kwani Inter Milan wataunyanyua rasmi kombe la Scudetto ya 2025-26 baada ya mechi ya mwisho ya msimu.
Hata hivyo, pozi aliyopiga Marcus Thuram ilikuwa ni heshima kwa picha maarufu ya gwiji wa NBA Kobe Bryant iliyopigwa mwezi Juni 2001, baada ya Los Angeles Lakers kuwashinda Philadelphia 76ers katika Mchezo wa 5 huko Philadelphia.