Marcus Thuram Atoa Heshima kwa Kobe Bryant Huku Inter Milan Wakitwaa Scudetto Yao ya 21.

Mshambuliaji wa Inter Milan Marcus Thuram alitoa heshima kwa gwiji wa NBA Kobe Bryant kupitia Instagram wakati akisherehekea ushindi wa Scudetto wa Nerazzurri.

Marcus Thuram Atoa Heshima kwa Kobe Bryant Huku Inter Milan Wakitwaa Scudetto Yao ya 21.

Nyota huyo wa Inter alirekebisha (recreate) moja ya picha maarufu za Kobe Bryant kwenye mitandao ya kijamii alipokuwa akisherehekea taji la 21 la Serie A ndani ya chumba cha kubadilishia nguo Jumapili.

Marcus Thuram alikuwa amefunga bao la kwanza katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Parma, ushindi uliowezesha Inter Milan kutwaa Scudetto wakiwa na mechi tatu mkononi.

Mara tu baada ya mechi, Thuram aliposti picha kwenye Instagram ikimuonyesha akiwa na mataji mawili ya Scudetto aliyoyashinda wakati wa kipindi chake katika Stadio Giuseppe Meazza.

Marcus Thuram Atoa Heshima kwa Kobe Bryant Huku Inter Milan Wakitwaa Scudetto Yao ya 21.

 

Ilikuwa ni picha iliyohaririwa, kwani Inter Milan wataunyanyua rasmi kombe la Scudetto ya 2025-26 baada ya mechi ya mwisho ya msimu.

Hata hivyo, pozi aliyopiga Marcus Thuram ilikuwa ni heshima kwa picha maarufu ya gwiji wa NBA Kobe Bryant iliyopigwa mwezi Juni 2001, baada ya Los Angeles Lakers kuwashinda Philadelphia 76ers katika Mchezo wa 5 huko Philadelphia.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.