Rais wa Napoli Aurelio De Laurentiis ana sababu ya kweli ya kuwa na wasiwasi kwani klabu hiyo inaonekana kukosa zaidi ya €100m katika mapato yanayowezekana.
Partenopei wamekuwa katika hali ya mtafaruku katika kipindi cha miezi sita kufuatia mafanikio yao ya Scudetto, wakiwatimua Rudi Garcia na Walter Mazzarri katika kipindi cha miezi michache iliyopita kufuatia kuzorota sana kwa fomu na matokeo. Kocha wa Slovakia Francesco Calzona kwa sasa anaongoza hadi majira ya joto.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa.
Napoli walishindwa tena kupata ushindi katika pambano lao na Cagliari Jumapili, wakilazimishwa sare ya 1-1 na kikosi cha Claudio Ranieri. Timu hiyo sasa inashika nafasi ya tisa kwenye msimamo wa ligi, pointi 11 nyuma ya Bologna iliyo nafasi ya nne.
Kama ilivyoripotiwa na Corriere dello Sport kupitia TMW, Napoli sasa wako mbioni kukosa Ligi ya Mabingwa na Kombe la Dunia la Vilabu, mashindano ambayo huleta mapato ya zaidi ya €100m kwa vilabu vinavyoshiriki.
Pia meridianbet inatoa michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.
De Laurentiis anatamani klabu hiyo kufuzu kwa aina fulani ya mashindano ya kimataifa, hataki klabu hiyo kukosa kabisa michuano ya Ulaya.