Vyanzo mbalimbali nchini Italia vinadai kuwa SSC Napoli wamekasirishwa na huenda wakachukua hatua za kinidhamu dhidi ya Romelu Lukaku, ambaye ameamua kufanya mazoezi Belgium hadi wiki ijayo bila idhini ya klabu.

Romelu Lukaku, mchezaji wa kimataifa wa Belgium, hajarejea Naples kama ilivyotarajiwa ili kuanza mazoezi leo asubuhi.
Vyanzo kadhaa, vikiwemo Sky Sport Italia, Il Mattino na La Repubblica, vinaripoti kuwa Lukaku alitakiwa kurejea kwenye kituo cha mazoezi cha klabu baada ya kumjulisha kocha wa timu ya taifa ya Belgium, Rudi Garcia, kuwa hakuwa fiti kucheza dhidi ya Mexico na United States men’s national team katika mechi za kirafiki za kimataifa wakati wa mapumziko, na alihitaji muda zaidi kurejea kwenye kiwango chake cha utimamu wa mwili.
Kwa mujibu wa Sky, Lukaku hayuko tayari kurejea Naples kabla ya wiki ijayo. Alitarajiwa kurejea leo asubuhi ili kuendelea na mazoezi chini ya msaidizi wa Antonio Conte, Cristian Stellini, huku Conte mwenyewe akiwa amechukua mapumziko mafupi na anatarajiwa kurejea Naples katika siku zijazo.


