Szczesny: "Juventus Hawakutaka Kurudia Kosa Lilelile"

 

Wojciech Szczesny anasema Juventus walikubali kwamba hawataweza kupoteza dhidi ya Atalanta kitu ambacho hawakuwa wamefanya dhidi ya Sassuolo wiki iliyopita.

 

Szczesny: "Juventus Hawakutaka Kurudia Kosa Lilelile"

Bianconeri walipata pointi moja kwenye Uwanja wa Gewiss jana kwa kupata sare ya 0-0 dhidi ya Atalanta.

Aviator, poker, Roullette, Wild Icy Fruits, Piggy Party na mingine kibao upige pesa na Meridianbet. Ingia www. meridianbet.co.tz.

“Siku zote tunacheza ili kushinda, hivyo tunapotoka sare, huwa tunapoteza pointi mbili. Nadhani yalikuwa matokeo ya haki hata hivyo, tulicheza vizuri zaidi katika kipindi cha kwanza, walikuwa bora zaidi kipindi cha pili. Wakati fulani, tulielewa hatukupaswa kupoteza mchezo na tuliteseka kidogo katika dakika kumi za mwisho.” Szczesny aliiambia DAZN.

Szczesny: "Juventus Hawakutaka Kurudia Kosa Lilelile"

Hili ndilo kosa tulilofanya dhidi ya Sassuolo, ikiwa ni pamoja na Fede Gatti na mimi. Wakati mwingine lazima ukubali kutoa uwezavyo ili kupata pointi, leo tumefanya vizuri zaidi, tunasikitika hatukushinda, lakini kama nilivyosema, ni hatua muhimu dhidi ya timu yenye nguvu. Alisema Mlinda malngo huyo wa zamani wa Arsenal.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Poland aliokoa bao muhimu katika kipindi cha pili, na kuisaidia Juventus kurejea nyumbani na pointi moja mfukoni. Alipoulizwa aliwezaje kuokoa mkwaju wa faulo wa Luis Muriel, Szczesny alisema kuwa hajui lakini ilikuwa ni muhimu kuokoa mpira huo.

Beti na Meridianbet kwa odds kubwa na machaguo kibao, pia unaweza kubashiri mubashara.

Szczesny: "Juventus Hawakutaka Kurudia Kosa Lilelile"

Szczesny alisema kuwa anaamini kuna mengi ya kufanya ili kuboresha. Walicheza vyema dhidi ya Lazio katika kipindi cha kwanza, vizuri dhidi ya Udinese katika kipindi cha kwanza, lakini lazima wasimamie mpira vyema. Jana walifanya vizuri kipindi cha kwanza, lakini walibadilisha mfumo kidogo katika kipindi cha pili, kwa hivyo lazima wachukue hatua moja zaidi ili kuwa na ushindani zaidi.

“Ni Septemba tu, sasa tuna derby nzuri na mapumziko ya kimataifa, lakini tunajiandaa kwa mchezo mmoja kwa wakati mmoja.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.