Thiago Motta Kusaini Juventus Wiki Ijayo
Makala iliyopita
Kipaumbele cha Inter Sasa ni Golikipa
Makala ijayo
Tottenham Kuachana na Lo Celso
Juventus wako kwenye mchakato wa kuijenga klabu hiyo upya na kuirudisha kwenye ubora ambao imekua nao kwa miaka mingi, Kwani miaka mitatu ya hivi karibuni wameonekana kusuasua kuanzia kwenye ligi ya nyumbani mpaka kwenye michuano ya ligi ya mabingwa barani ulaya.
Kocha Thiago Motta ameiongoza klabu ya Bologna kwa mafanikio makubwa tangu akabidhiwe timu hiyo mwaka 2022, Hivo kwa miaka miwili aliyokuwepo klabuni hapo ameiwezesha klabu ya Bologna kufuzu ligi ya mabingwa ulaya msimu ujao ikiwa ni baada ya zaidi ya miaka 50 jambo ambalo limewavutia Juventus na kuona ni moja ya makocha ambao wanaweza kuifikisha timu hiyo mbali.