Piotr Zielinski ameaga rasmi Napoli baada ya miaka nane na barua ya wazi kwa mashabiki, huku akiondoka kama mchezaji huru na kujiunga na Inter.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Poland aliwasili kwa mara ya kwanza katika uwanja wa Stadio San Paolo, na baadaye kuitwa Stadio Diego Armando Maradona, kwa uhamisho wa €16m kutoka Udinese majira ya joto ya 2016.
Kabla ya hapo, alikuwa ametua Italia akiwa kijana katika akademi ya Udinese mwaka wa 2011 na pia alikuwa na kipindi cha mkopo na Empoli.

“Napoli… timu yangu Napoli…” aliandika Zielinski kwenye Instagram.
“Baada ya miaka 8, tunachukua njia tofauti … ulinikaribisha nilipokuwa mtoto na niliondoka kama mwanamume na baba. Naples ilikuwa nyumba yangu na daima itakuwa sehemu yangu na familia yangu… Nilipitia nyakati za kipekee na zisizofutika ambazo nitazihifadhi moyoni mwangu.”
Mchezaji huyo aliongeza kuwa, Napoli ilimpa marafiki wengi ambao watakuwa sehemu ya maisha yake milele. Anawashukuru MASHABIKI wa kipekee kwa moyo wao mkubwa. Wamemfanya ajisikie kuwa sehemu yake.

“Pamoja tulishinda vikombe muhimu… kisha Scudetto baada ya miaka 33. Ni furaha iliyoje kusherehekea kwa pamoja… Nitashukuru daima kwa JEZI hii!!. Naishukuru klabu iliyoniruhusu haya yote na wafanyakazi walionisindikiza katika safari hii. AHSANTE milele kutoka kwangu … ‘Napolacco’ ZIELU yako.”
Neno Napolacco ni muunganiko wa Napoletano na Polacco – Neapolitan na Polish – inayowakilisha utambulisho wa pande mbili wa Zielinski uliotengenezwa kwa miaka hiyo nane.


