Rasmi sasa Mabingwa wa soka la wanawake Tanzania, JKT Queens, wameandika historia nyingine kubwa ya kuvutia baada ya kutwaa taji la Mashindano ya CECAFA Women’s Championship 2025.
Mabingwa hawa wa CECAFA ndio timu pekee nchini Tanzania iliyofanikiwa kutwaa hili taji mara mbili tena ikiwa kwenye ardhi ya ugenini, wakiwaacha nyuma wenzao wa Simba waliofanikiwa kutwaa taji hilo mara moja.

Katika mchezo wa fainali uliofanyika jana dhidi ya Rayon Sports ya Rwanda, mabingwa hao walionesha ubora wao kwa kushinda bao 1–0. Goli la pekee la JKT Queens lilifungwa na Winnie Gerald.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Kwa ushindi huu sasa rasmi JKT Queens wamefanikiwa kufuzu kushiriki Ligi ya Mabingwa Afrika ya Wanawake (CAF Women’s Champions League) wakiwa wawakilishi rasmi wa ukanda wa CECAFA.


