Nahodha wa Manchester United na beki wa timu ya taifa ya Uingereza – [Harry] Maguire, ameondolewa kwenye kikosi cha Uingereza muda mfupi baada ya kupatikana na hatia ya makosa aliyoshitakiwa nchini Ugiriki.
Mapema wiki iliyopita, Maguire alishitakiwa kwa makosa ya kumtukana na kumpiga afisa wa polisi pamoja na vitendo vya rushwa wakati akiwa likizo pamoja na rafiki zake nchini Ugiriki.
Taarifa ziliripoti vitendo hivyo vilitokea baada ya mtu mmoja kumchokoza dada yake Harry na hivyo vurugu za maneno na vitendo kutokea katika visiwa vya Mykonos. Mapema siku ya Jumanne, wakili wa beki huyo alikanusha mashtaka hayo.
Jumanne jioni ilitoka taarifa ya Harry kuhukumiwa miezi 21 jela na hivyo kocha wa Uingereza kuchukua uamuzi wa kumuondoa beki huyo kwenye kikosi chake.
Maguire kukosekana kwenye Kikosi cha Uingereza.
“Kutokana na taarifa za hivi punde, ninathibitisha kumuondoa Maguire kwenye kikosi cha Uingereza kitakachocheza michezo dhidi ya Iceland na Denmark.
“Kama nilivyosema mwanzoni, nilikuwa ninaliangalia jambo hili linavyokwenda. Baada ya kuzungumza na Manchester United pamoja na mchezaji mwenyewe, nimefikia uamuzi wa kumuondoa Harry Maguire kwenye kikosi kwa maridhiano ya pande zote na kwa ajili ya maandalizi kuelekea michezo hiyo.” amesema Kocha wa Uingereza – Gareth Southgate.
Beti Mbio za Mbwa Mubashara
Hii ni rahisi zaidi! Hapa USHINDI unaupata kwa kuchagua mbwa anayeshinda mbio na machaguo mengine yenye odds tamu.
Ester jackson
Nidhamu nj muhimu sana katika mchezo na jamii inayokuzunguka sheria ifuate mkondo wake pale wanapofanya kosa
rama
maguire anaweza kushuka kiwangona thamani yake kibiasha anatakiwa ajilekebishe atari sana hiii upande wake
Adelta
Nidhamu Ni kitu muhimu sana ktk jamii inayokuzunguka na popote unapokuwa@meridianbettz
Mwanahamisi
Nidhamu ni Jambo muhimu sana katika wachezaji
Mwajumah
Nidhamu Ni muhim sana katika michezo shelia ifuate mkondo wake pale wanapofanya kosa#Meridianbettz
Khadija
sheria ifate mkondo wake pale panapokuwa na kosa
Fatina mfingi
Nidhamu Ni Jambo njema kwa Kila mchezaji kwaiyo acha Sheria ifate mkondo wake ili iwe funzo kwa wengine!
Caroline
Ni vizuri ajifunze kua na nidhamu
Tatu
Maguire alikosa heshima na nidhamu nje ya kazi na ndani ya kazi adhabu aliyopewa anastahili
Zeiyana
Kwa kumuangalia Maguire huwani kabic na kitendo alicho fanya me naona ilikua asila tu daaah…!
Sauda
Itakuwa fundisho kwa wachezaji wengine
Dorophina
Wamefanya vizuri wakimuongezea na adhabu nyingine ili iwe fundisho kwa wengine
Sylvester
England watakua na pigo kubwa kwa kukosekana kwa Maguire kwani kwa sasa ni kiongozi mkubwa kwenye ngazi ya klabu na Taifa inabidi wakate rufaa ili kesi hyo isikilzwe tena
felister
itakua fundisho siku nyingine kwake na wengine
Rehema
Ni kheri ajifunze nidhamu
Fatuma kasomo
Nidhamu muhimu
Nasra
Itakuwa fundisho sana
aisha
Ni vizuri ili ajifunze heshima na ikumbukwe kila mtu nilazima ajue yeye ni nani na kwanini yupo hapa duniani na akitoka hapa duniani ataenda wapi
Gabriel
Kitendo alichoamua Gareth Southgate kocha wa uingereza kwa kumtoa maguire sio mbaya maana kwanza ameangalia nidhamu ya timu na pia kingemfanya magu asicheze kwa Uhuru maana kwa tukio hilo amefanya kwa hasira
Issa
Waingereza wanakosea kumuacha huyu beki sasa watamuweka nani pale
Neema
Nidhamu ni jambo la msingi sana.
Sadick
Sijui nini kimemupata Harry Maguire na nduguze kupigana na polisi na kujaribu kutoa rushwa na mwisho wa siku ameadhibiwa baada ya kupatikana na makosa yote hayo, kwa mtu mwenye jina kubwa kama yeye alipaswa kujizuia#meridianbettz
farida ahmadi
Lazima hatua za kisheria zifate mkondo wake
Shan
Parfomance yake haikuwa vizuri msimu ulioisha.
Latifa juma mohamed
Maguire anaweza kushuka kiwango na pia anajishusha utu , haikuwa haha ya yye kutakan ni muhimu tu angefanya funika kombe mwanaharamu apite.
Saupha mohamed
Ilo ni fundisho
Hope mwaikuka
Ndo faida ya kutokua na nidham
Rose kapinga
Hili ni funzo kwa wengine!!!
Povel
Sheria imefuata mkondo wake
Sabrina
Duuh Kweli ni mtovu wa nidhamu haki yake kufukuzwa
Amiri Kayera
Dah hii issue imemchafua sanaa
Shafii
Hakua kwenye wakati mzuri ndani ya club ya man u 2020/2021 sababu hiyo imepelekea asiitwe kwenye kikosi cha uingereza.
Lydia Emmanuel Magoti
Duu Nini Sasa aundio ukosefu wanidhamu jamani
Ernest
Kashfa mbaya sana kwa Maguire
Furahav
Majanga
David Pere
Nidhamu Ni muhim sana katika michezo shelia ifuate mkondo wake pale wanapofanya kosa
magdalena
kosa alilolifanya ni kubwa sana ila kwa sisi mashabiki wa united tunabaki mikono tumeweka katika mashavu
warda
Dooo pole yake sana
Samiah
Balaa zito
Devotha
Pole yake iwe funzo na kwawengine