Kijana machachari kutoka Southampton, Sam McQueen rasmi sasa anajiunga na Middlesbrough. Kijana huyo mwenye umri wa miaka 23 ni zao kutoka katika mfumo wa vijana wa Southampton, anauwezo wa kucheza mbele na nyuma upande wa kushoto.
McQueen anajiunga kwa Middlesbrough kwa msimu mzima kwa mkopo, ameichezea Southampton mara 50 mara 20 kati ya hizo ni ligi ya Premier. Mchezo wake mkubwa wa kwanza ulikuwa katika ligi ya EUROPA miaka miwili iliyopita. anakuwa kijana wa sita kusajiliwa kwa mkataba wa kudumu, anaungana na Aden Flint, Paddy McNair, Andy Lonergan , Jordan Hugill na Mo Besic McQueen anatarajiwa kuvaa jezi namba 14 msimu huu.
Povel tz
Gud news
Issa
Habar nzuri
Fatina mfingi
Asanteh kwa taarifa meridianbet!!