Kinda wa Juventus Moise Kean ameandika rekodi mpya kwenye Ligi ya Italia -Serie A baada ya kuwa mchezaji mdogo zaidi kufunga magoli kwenye mechi 4 mfululizo za Serie A, ameifuta rekodi iliyoandikwa na Mio Balotelli.
Staa huyu mara nyingi amekuwa akifananishwa na Mario Balotelli ambaye alifunga magoli kwenye mechi 3 mfululizo mwaka 2009.
Mkwaju uliotandikwa na Joao Cancelo ulionekana kulilenga goli, lakini golikipa alikuwa mbioni kuunasa huku kijana Moise Kean akimvuruga kipa kwa kumkwepeshea mpira huo.
Kama Juve wakishinda gemu dhidi ya SPAL watakuwa wamejiandikia ubingwa mwingine wa Serie A kwa miaka 8 mfululizo. Kean anakuwa muhimu mno wakati kama huu wakati mastaa kama Cristiano Ronaldo akikosa gemu 2 kwa sababu ya jeraha.
Kinda huyu wa miaka 19 pia amefanya makubwa katika timu ya Taifa ya Italia mwaka huu akifanikiwa kucheka na nyavu kwenye gemu ya kufuzu Euro 2020 wakati wa likizo ya kimataifa.
Furahav
Kean noma sana.
Povel
Habar njema
Issa
Moise kean ni noma