KisaΒ ya kwanza cha Covid-19 kimepatikana katika kijiji cha wanamichezo na mtu aliyeathiriwa ni kutoka nje ya nchi na anajulikana kama “Wafanyakazi wanaohusika na Michezo” na amewekwa katika karantini ya siku 14, waandaaji walisema hapo awali kijiji cha Olimpiki kitakuwa “mahali salama zaidi” huko Tokyo; Olimpiki zilizocheleweshwa kuanzia Julai 23 hadi Agosti 8.
Afisa huyo amekuwa mkazi wa kwanza katika kijiji cha wanamichezo wa Olimpiki ya Tokyo kukutwa na maambukizi ya Covid-19, waandaaji wa Michezo walithibitisha siku ya Jumamosi.
Mtu aliyeathiriwa kutoka ugenini alipimwa na hakuwa na maambukizi wakati wa kuwasili Japani lakini baadaye akapimwa akakutwa na maambukizi katika vipimo vilivyochukuliwa katika mchakato wa uchunguzi ndani ya kijiji.
Habari hiyo italeta wasiwasi mkubwa kwa waandaaji ambao hapo awali walisema Kijiji cha Olimpiki kitakuwa “mahali salama zaidi” huko Tokyo.
Olimpiki ya Tokyo 2020, iliyoahirishwa kwa mwaka kwa sababu ya janga la ulimwengu, inafanyika zaidi bila watazamaji na chini ya sheria kali za karantini kutoka Julai 23 hadi Agosti 8.
Tokyo ilirekodi maambukizI mapya 1,271 jana – siku ya tatu moja kwa moja ambapo idadi hiyo imezidi 1,000.
Ndio, kama bado hujajiunga na Familia ya Mabingwa ya Meridianbet, huu ndio wakati wako! Tunakupatia Bonasi ya 3,500 Tsh papo hapo kama sehemu ya ukaribisho!