Juan Roman Riquelme Legendary Atakae Kumbukwa na Boca Juniors

Unahitaji kuwa na shilling 450 za kitanzania, kutoka katikati ya Jiji la Buenos Aires mpaka San Fernando de la Buena Vista , mitaa hii imemlea RiqueBaller Juan

Jioni moja katikati ya miaka ya 90 Kocha wa Boca Juniors, Bwana Carlos Salvador Bilardo alitembelea mitaa hii mitakatifu kabisa ya soka, ghafla macho yake yalitua kwa Juan mwenye miaka 16 tu na namba 10 mgongoni, akitandaza mpira anavyotaka yeye, juu ya vumbi na tambaa la Unahodha

Roman Riquelme

Bilardo alisogea pembeni na kumuuliza kijana mmoja “Quien es ese” kijana alimjibu “Es decir Diego Maradona”Jamaa alichoka sana, yani aliuliza yule nani, ila kijana akamwambia yule ni Diego Maradona, yani kuna mitaa ya Argentina ina Maradona mwingine uwanjani na anakipiga

Ilikua mchakato wa haraka sana, kwa Boca Juniors kupambana kuipata saini yake kutokea Argentino Junios, na pale La Bombonela ilikua balaa sana, walimpa jezi na akiwa na miaka 18 tu, moto uliwaka sana uwanjani, alicheza namba 10, akicheza kama hataki ila ufundi mwingi mno

Miaka ya 2000 wale Barcelona hawakutaka kabisa kumuelewa kocha wao Luis Van Gaal, alikataa usajili wa Juan ila bodi ilimpinga, unamuachaje Maestro kama yule, wakamleta Barca ila LVG akauita usajili wa kisiasa na kuamua kumtia bench

Maradona wa San Fernando alikula sana mkeka pale Nou Camp, ila kila akipewa namba anachezeshwa winga ila alikua bado fundi mno, anatokea pembeni na kijiji chake na kutupia sana, akapewa Mwenyekiti wa Kijiji cha Mawinga wote Spain

Maisha yake yalitakata baada ya kwenda kwa Nyambizi wa njano, Villareal ndipo hapo miguu ya almasi na akili ya kioo ikafahamika duniani kote, alichezeshwa kama Central Midfielder, alikuwa na Orchestra moves yani miondoko kama vinanda vya Tuddy Thomas anafunga kutokea kati na kuchezesha mno

Inaaminika ni namba 10 ya mwisho asili duniani, mikononi mwake ana tuzo za mchezaji bora wa mwaka Argentina mara nne, alizaliwa tarehe 24-06-1978 siku moja kabla Argentina ajabeba kombe la dunia, FALTA MAGICIA, FALTA ROMAN

16 Komentara

    Moja Kati ya vizaz vilivyofany vzr katika ilimwengu wa soka na wameacha doa mpka leo hawajasaulika

    Jibu

    Huyu jamaa nilikuwa simuelewi lakini alikuwa fundi

    Jibu

    LVG alizingatia sana taaluma yake bila kujali mashabiki au viongozi wanasemaje! Thanks meridian kutujuza

    Jibu

    Anajua jamaa.

    Jibu

    What a Legendary!!! One of the greatest player of his time.

    Jibu

    Yuko vizuriii

    Jibu

    Amefanya kaz kubwa sana kwny soka

    Jibu

    Yuko Poa sana

    Jibu

    Alikuwaga tishio

    Jibu

    Yuko vizuri Sana

    Jibu

    Yupo poa sana

    Jibu

    Yuko vzur sana

    Jibu

    ametsha

    Jibu

    Yuko vizuri Sana..

    Jibu

    namkubali sana

    Jibu

    Yuko pouw

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.