Olivier Giroud Hadi Sasa tunavyosoma hii habari ndani ya msimu huu wa 2020/21 amecheza Michezo 3 pekee,akitumia dakika 33 tena kwa kutokea benchi ila kiujumla kwenye mashindano yote ambayo Chelsea wapo amecheza dakika 154 Michezo 6 goli 1, hiki kitu kinampa mawazo na inasemekana huenda akaondoka BAADA ya mkataba wake kuisha mwakani mwezi wa 6.
Huyu mwamba Olivier Giroud alijiunga na Arsenal mwaka 2012 akitokea Tours fc ya Ufaransa ambayo alikuwa kwa mkopo akitokea Montpelier fc kwa dau linasadikiwa kuwa (Euro 12.4mil) akidumu Arsenal Hadi 2018 akaamua kwenda kutafuta marisho mapya pale kwenye Viunga vya Roman Abrahimovic, akiwa na The Blues mwamba amefanikiwa kushinda mataji kadhaa ikiwemo Europa League mwaka 2018/19 na kuwa mfungaji bora wa mashindano akifunga magoli 11.
Olivier Giroud na Rekodi za FA
Mimi huwa namuita Olivier Giroud Mr. FA Cup Winner, inawezekana ndio mchezaji wa kifaransa kwa miaka ya hivi karibuni aliyeshinda mataji mengi ya FA uingereza kwani amebeba Mara 4,lakini Mara 3 akiwa na Arsenal (2014,2015 na 2017) na Chelsea (2018) lakini TAYARI huyu binadamu ana taji la kombe la dunia la mwaka 2018 na Timu ya taifa ya Ufaransa,ameshiriki Mara mbili michuano ya kombe la dunia 2014 Brazil na 2018 Russia walipofanikiwa kubeba ndoo, huyu bwana mwaka 2009/10 alikuwa mfungaji bora huko Ligi Daraja la pili akifunga magoli 21 haitoshi akaja Ligi kuu Ufaransa akaweka goli 21 msimu 2011/12 nakuwa mfungaji Bora huku Montpelier wakitwaa taji la Ligi.
Jaribu sasa hapa Meridianbet. Ukiacha ukweli kuwa itakupa burudani maridadi, bado inakuhakikishia ushindi mkubwa. Kazi kwako kukusanya ushindi!
magdalena
dah wanakosea kumuweka benchi kipaji chake kimpira kitashuka sana na kuumuia ni muhimu
Carolyn
Sawaaaa
warda
Asepe tu ni mda mrefu kakaa chelsea
Sauda
Benchi siyo poa kabisa
zeiyana
chelsea hawawezi kumuacha haende olivier bado hana msaada mkubwa clabuni hapo
Povel
Giroud Hana nafasi tena kwny kikos cha chelsea natumai January anawez kusepa nakutafuta timu ya kupata nafasi ya kucheza kikos cha kwanza
Tatu
Mm naisi Chelsea awamtaki kwa sasa
Dorophina
Olivier naona kama hana msaada na chelsea ni bora akae benchi tu
aisha
Duuuh chelsea noma sana
Issa
Girooud falsafa ya lampard kama inamshinda na umri pia tatizo
Saupha mohamed
Dhuuu nomaaa sana
Sabrina
Duuh hatari
Hopemwaikuka
Imekaa vibaya hii
Johnmary jo
Ee jamani maamuzi ni ya viongozi wake kumuacha au kumuongezea muda#meridianbett
Fatina mfingi
Mmh itakuwa ss
Mwajumah
Aende zake tu kwani ni muda mrefu kakaa chelsea
Khadija
Aende tuu kwan kaaa sana hapo
Elika
Kila la kheri huko aendako
Ester jackson
Yan huyo tumeshamchoka atimuke tu tunasubiri dirisha dogo la usajili tumuweje sokoni wanachelsee
Nasra
Giroud umr umesonga na atundike daluga
Shani
Aende tu akamaizie mpira kwengine
Rahma
Kila lakheri