Mabingwa wa LaLiga, FC Barcelona, wamehitimisha msimu wa ligi wakiwa na rekodi ya kushinda mechi zote za nyumbani kwa mara ya kwanza tangu msimu wa 1959/60 baada ya kuifunga Real Betis mabao 3-1 katika dimba la Camp Nou.
Barcelona walionekana kutawala mchezo tangu mwanzo, huku mashambulizi yao yakiiweka Betis katika presha kubwa. Wageni walifanikiwa kupeleka mpira wavuni dakika ya 23 kupitia Abde Ezzalzouli, lakini bao hilo lilikataliwa kutokana na kuotea.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Dakika chache baadaye, Raphinha aliipa Barcelona bao la kuongoza baada ya kupiga mpira wa adhabu uliomshinda kipa Álvaro Valles. Betis walijaribu kusawazisha kupitia mashambulizi yao, lakini walikosa umakini mbele ya lango.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ya chini huku Isco akiingia na kujaribu kuongeza nguvu katika safu ya ushambuliaji ya Betis. Hata hivyo, kosa kubwa la Héctor Bellerín lilimpa nafasi Raphinha kuongeza bao la pili kwa shuti la chini lililojaa wavuni.
Betis walipata matumaini baada ya kupewa penalti yenye utata dakika 20 kabla ya mchezo kumalizika, ambapo Isco alifunga bao lake la kwanza msimu huu. Antony alikaribia kusawazisha kwa shuti kali lililopita karibu na lango, lakini João Cancelo alihitimisha ushindi wa Barcelona kwa bao zuri la shuti la mbali.

Ushindi huo unaifanya Barcelona kuendeleza ubabe wao dhidi ya Betis kwa kupata ushindi wa 12 katika mechi 15 za mwisho walizokutana, huku kocha Manuel Pellegrini akiendelea kushikilia rekodi ya kufungwa mara nyingi zaidi na miamba hiyo ya Catalonia.


