Kuelekea Januari 24, 2021 – mbio za kuwania uraisi wa klabu ya Barcelona FC unashika kasi! Hii ni baada ya wagombea waliopita kwenye hatua ya kwanza kubaki wanne tu.
Mchakato wa kumpata raisi mpya wa klabu hiyo ulianza tangu 2020 kabla na baada ya raisi Bartomeu kujiuzulu nafasi yake ya kuiongoza Barcelona.
Kati ya majina ya wagombea waliotia nia ya kukamata usukani wa klabu hiyo ni Joan Laporta, Victor Font, Toni Freixa na Emili Rousaud waliosalia kwenye mchakato wa uchaguzi.
Kwa taratibu za uchaguzi, wagombea wote walipaswa kupata saini za wanaowasapoti huku idadi ya chini iliyowekwa ikiwa ni kura 2,257. Kwa idadi hiyo, Laporta amepata saini 10,272, Font (4,713), Freixa (2,822) na Rousaud (2,510).
Utaratibu wa kuhakiki saini hizi utafanyika leo (Jumanne) na matokeo ya watakaoidhinishwa yatatangazwa Alhamisi wiki hii.
Licha ya kuwa na mapendekezo ya kubadilisha tarehe ya uchaguzi kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo COVID19, Barcelona wameendelea kusisitiza Januari 24 itabaki kama ilivyopangwa hii ni baada ya taratibu zote za uchaguzi kukubaliwa na mamlaka zote zinazohusika.
MERIDIANBET INAKUPA NAFASI YA KUWA MILIONEA KWA KILA BAADA YA DAKIKA 5
Mchezo wa Keno unakupatia fursa ya kuibuka kidedea kupitia droo zinazochezwa kila baada ya dakika 5 tu!! Tunaposema Meridianbet ni nyumba ya mabingwa, tunamaanisha!!
Sania
Uchaguzi umepamba moto
Salma ngende
Kumenoga
Magdalena
Ngoja tusubiri wakati ujibu
Shakila mrope
Atariatari
Hopemwaikuka
Tunamsubr mshnd
Caroline
Good news
Dorophina
Uchaguzi unaendelea kupamba moto
Gabriel
Habari njema
Janeflora malisa
Asnt kwa taarif meridianbet
aisha
Safi sana
Ernest Kimeru
Ngoja tuone
Saupha mohamed
Goodnews
Lydia Emmanuel Magoti
Atariii hapo
Sarah
Habari njema
Sabrina
Taarifa zimetulia
warda
pole yao