Camavinga Aongeza Mkataba Mpaka 2029

Kiungo wa klabu ya Real Madrid na timu ya taifa ya Ufaransa Eduardo Camavinga amefanikiwa kuongeza mkataba wa kuendelea kusalia ndani ya klabu ya Real Madrid mpaka mwaka 2029.

Eduardo Camavinga alikua bado ana mkataba ndani ya klabu ya Real Madrid lakini amefanikiwa kuongeza mkataba mwingine ambao utamuweka klabuni hapo mpaka mwaka 2029.camavingaKlabu ya Real Madrid imeweka kiasi cha Euro bilioni moja kwa klabu ambayo itahitaji saini ya mchezaji huyo, Hivo ni wazi klabu hiyo haifikirii kumuachia mchezaji huyo.

Real Madrid inawaongezea mikataba mirefu wachezaji wake wadogo kwa kile kinachoelezwa kutengeneza kizazi kipya kitakachodumu kwa muda mrefu zaidi ya timu hiyo kama ambavyo kizazi kilichopita kimefanya.camavingaToni Kroos, Luca Modric, na wachezaji wengine wenye umri mkubwa wako mbioni kutimka klabuni hapo, Hivo Real Madrid imewaongezea mikataba wachezaji kama Federico Valverde, Camavinga, Rodrygo, Vinicius Jr, Tchouameni ambao wanatarajiwa kutengeneza kizazi kipya cha klabu hiyo na kuleta mataji klabuni hapo.

 

 

 

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.