FC Barcelona tayari wamehakikisha ubingwa wa La Liga kihesabu, lakini bado wana mechi tatu za kucheza kabla msimu wa ligi wa 2025-26 kumalizika rasmi. Katika michezo hiyo, Blaugrana watakuwa wakilenga kufikisha pointi 100.
Mchezo wa kwanza kati ya hiyo unatarajiwa kuchezwa usiku wa leo, Jumatano, dhidi ya Deportivo Alavés katika uwanja wa Mendizorroza Stadium. Klabu hiyo ya Catalonia tayari imetangaza kikosi cha mchezo huo, huku kukiwa na baadhi ya mabadiliko kwenye orodha hiyo.
Beki Andreas Christensen amerejea kwenye kikosi baada ya kupona jeraha la muda mrefu lililomuweka nje tangu mwishoni mwa mwaka jana. Kwa upande mwingine, Fermín López na Frenkie de Jong wameachwa nje kwa sababu za kiufundi, huku Raphinha akisuspishwa kwa mchezo huo kutokana na kufikisha idadi ya kadi za njano.
Kikosi kamili kilichotangazwa na FC Barcelona ni kama ifuatavyo: