Javier Mascherano Amestaafu Kucheza Soka.

Waswahili husema ‘kila chenye mwanzo, hakikosi kuwa na mwisho’. Kama ilivyokuzaliwa, kuna kufa. Javier Mascherano ametundika daruga kwenye ulimwengu wa soka la kulipwa.

Mashabiki na wadau wa mchezo wa soka wanafahamu ukubwa wa jina Javier Mascherano. Uwezo wake wa kuongoza safu ya ulinzi katika vilabu vikubwa kama Barcelona na Liverpool pamoja na timu ya taifa ya Argentina, utaendelea kukumbukwa daima.

Mascherano alitangaza kustaafu kucheza soka la kulipwa baada ya kuwa uwanjani kwa miaka 17.

Mascherano wakati anaitumikia Liverpool

Katika historia ya Argentina, Mascherano ndio mchezaji aliyecheza michezo mingi (147) akiwa na timu ya taifa hilo. Mwezi Januari, Mascherano aliamua kurudi nyumbani na kusajiliwa na timu ya Estudiantes de La Plata.

Baada ya kupoteza mchezo dhidi ya Argentinos Juniors kwa matokeo ya 1-0, Mascherano (miaka 36) alisema ni muda sahihi wa kuachana na soka.

“Ninataka kutangaza leo ninastaafu kucheza soka la kulipwa. Ninaishukuru klabu hii kwa kunipatia fursa ya kumaliza maisha yangu ya soka nikiwa Argentina.

“Niliitumikia taaluma yangu kwa 100% na nilifanya kila nililoweza. Leo nimegundua muda mwingine inakuwa ngumu kwangu na sitaki kuwavunjia heshima Estudiantes walioniamini na kunirudisha Argentina au wachezaji wenzangu au taaluma ya soka.” alisema Javier Mascherano.

Mascherano akiwa River Plate.

Mascherano aliianza safari ya kucheza soka akiwa na klabu ya River Plate kabla ya kutimkia Corinthians kisha alijiunga na West Ham United na mwaka 2007 alisajiliwa na Liverpool.

2010 alijiunga na Barcelona ambapo alipata mafanikio makubwa zaidi alipokuwa Camp Nou. Alibeba mataji 5 ya LaLiga na 2 ya Ligi ya Mabingwa – UEFA kati ya mengine mengi.

Mascherano Alipokuwa Barcelona

Mascherano aliisaidia Argentina kufika fainali ya Kombe la Dunia 2014 ambapo walifungwa na Ujerumani kwenye dakika 30 za nyongeza. Walimaliza nafasi ya pili mara 4 kwenye Copa America na kubeba medali mbili za dhahabu kwenye Mashindano ya Olympic.

Baada ya kuitumikia Hebei China Fortune kwa miaka miwili, Javier Mascherano alirudi nyumbani na  kujiunga na Estudiantes ambayo aliitumikia mpaka alivyotangaza kustaafu siku ya jana (Jumapili).


BASHIRI UKIWA MAHALI POPOTE!

Hauhitaji kuwaza linapokuja suala la ubashiri na odds kubwa. Bashiri na Meridianbet ukiwa popote ufurahie ushindi mkubwa katika michezo mbalimbali na hadi milioni 16 kwenye michezo ya kasino.

Meridianbet Beti Popote

INGIA MCHEZONI!

21 Komentara

    astaafu tu katumikia sana soka umri umeenda apumzike sasa

    Jibu

    Bora apumzike tu

    Jibu

    Mapumziko mema..

    Jibu

    Safi sana kazi na umri mapumziko mema

    Jibu

    Apumzike tu

    Jibu

    Mashabiki tunakutakiya Kila la kheri kwa kustafu

    Jibu

    Kila laheri kwenye maisha mampya

    Jibu

    Hamafanya kazi kubwa kwenye ulimwengu wa soka javier historia yake haiwezi kufutika

    Jibu

    Vizuri Sana umeitumia kazi yako kiufasaa kustafu kwako pongezi zako pumzika tuuu jembee

    Jibu

    All the best

    Jibu

    Sio mbaya pumzka sasa

    Jibu

    Mapumziko mema

    Jibu

    Haina ubishi kwamba Jevier alijitoa mno kwa timu alizochezea na hata kauli yake ya kustaafu inadhirisha uaminifu wake

    Jibu

    Javier pumzika kwa amani tutaenzi uhodari,kujituma,na mazuri yote ukifanya katika ulimwengu wa soka

    Jibu

    Mpira kautendea haki javier masherano

    Jibu

    Kazi na umri babu pumzika tu

    Jibu

    Atakumbukwa sana jinsi alivyocheza soka

    Jibu

    Apumzike salama

    Jibu

    Bora iwe hvyo

    Jibu

    Bora apumzike

    Jibu

    Muda wake umefika awapishe na wengine tuone vipaji vyao nenda tu kapumzike

    Jibu

Acha ujumbe