Wiki imezidi kuwa mbaya ya Real Madrid baada ya kupoteza mchezo wa jana kwa bao 1-0 wakiwa ugenini dhidi ya Valencia ambao wanashikilia nafasi ya 13 kwenye msimamo wa ligi kuu ya Hispania.

 

Madrid Yashindwa Yachapika Ugenini, Huku Vini Akipewa Kadi Nyekundu

Siku nne baada ya kuchapwa na Manchester City kwenye Ligi ya Mabingwa na kuondolewa kwenye Kombe hilo kama Mabingwa watetezi na jana pia wameshindwa kunyakua ushindi.

Mechi hiyo iligubikwa na malalamiko zaidi ya unyanyasaji wa kibaguzi yaliyoelekezwa kwa Vinicius Junior, na mchezo ulisimamishwa kwa muda baada ya Mbrazil huyo kuonekana kuwaonyesha wahalifu kwenye umati.

Kisha alionyeshwa kadi nyekundu ya moja kwa moja kwa kumzomea Hugo Duro dakika za nyongeza 90+7.

Madrid Yashindwa Yachapika Ugenini, Huku Vini Akipewa Kadi Nyekundu

Matokeo hayo yalipunguza hofu ya Valencia ya kushuka daraja LaLiga huku Madrid ikishuka hadi nafasi ya tatu nyuma ya wapinzani wa jiji hilo Atletico Madrid, ambao waliwashinda Osasuna 3-0 kwa mabao ya Yannick Carrasco, Saul Niguez na Angel Correa.

Espanyol walijipa uhai katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Rayo Vallecano huku Seville derby ikiisha kwa sare tasa kati ya Sevilla na Real Betis, ambao Juan Miranda alitolewa nje kwa kadi nyekundu.

JIBU

Tafadhali andika maoni yako
Tafadhali andika jina lako hapa