Tofauti Ya Alama 3 tu La Liga!

Ligi Kuu ya Hispania, La Liga imepamba moto sasa, huku timu tatu zinazoongoza ligi hiyo, Atletico Madrid, Barcelona na Real Madrid wakipishana kuongoza usukani wa ligi hiyo kwa alama tatu tu!

Atletico Madrid wanaongoza ligi hiyo wakiwa na alama 66, huku Barcelona wakiwa nafasi ya pili na alama 65 na vijana wa Zidane wakiwa na alama 62, wakiwa wemecheza michezo sawa 29.

Atletico Madrid waliongoza ligi hiyo kwa alama zaidi ya kumi lakini baada ya hapo wamekuwa wakifanya na vibaya huku wakiwapa nafasi Barcelona na Madrid kuwafikia. Hii inajumuisha mchezo wao wa mwisho ambao walifungwa na Sevilla 1-0 wakiwa nyumbani.

Barcelona walishinda 1-0 dhidi ya Villadolid hapo jana na goli likiwekwa kambani na Ousman Dembele dakika za mwisho kabisa, huku Villadolid wakiwa punguzu baada ya mchezaji wao kupewa kadi nyekundu.

Real Madrid wao walishinda 2-0 mchezo wao wa mwisho dhidi ya Eibar, magoli yakifungwa na Marco Assensio na Karim Benzema. Wikiendi hii kutakuwa na EL CLASSICO na kumekuwa na presha kubwa sana kutokana na msimamo ulivyo.

Je, nani ataongeza ligi hiyo? Endapo Diego Simione atashindwa kuchukua ubingwa msimu huu afukuzwe Atletico Madrid?


INAWEZEKANA KUWA MILIONEA BILA KUVUJA JASHO NA KASINO YA ODD ONE OUT.

Odd One Out kutoka Meridianbet ni moja ya kasino maridhawa yenye picha halisi, ambayo inakupa nafasi ya kushinda kadri uwezavyo na kuwa milionea mara baada ya mzunguko kukamilika.

CHEZA HAPA

4 Komentara

    Safi

    Jibu

    Iko vizuri Sana

    Jibu

    Safii

    Jibu

    Nawaombea Madrid washike usukani

    Jibu

Acha ujumbe