Zimwi likujualo, halikuli likakwisha. Ndicho kinachokwenda kuwatokea Dar es Salaam Young Africans – Yanga SC.
Baada ya kutemana na Hamis Tambwe, 2018/19. Klabu hiyo ilishtakiwa kwa kutomlipa Tambwe Stahiki zake kama ambavyo alistahili. Kwa mujibu wa kesi hiyo ambayo ilielekezwa Fifa, Yanga walipaswa kumlipa mchezaji huyo takribani milioni 43.5.
Fifa iliielekeza klabu hiyo kumlipa Tambwe na klabu ilikata rufaa ya maelekezo hayo na kupeleka sakata hilo kwenye mahakama ya kimichezo – CAS, nchini Uswisi.
CAS nayo ilitoa tamko la kuitaka klabu hiyo kumlipa Tambwe kama ambavyo Fifa ilielekeza hapo awali.
Tambwe alirudisha suala hilo Fifa akiomba msaada zaidi na kwa mujibu wa wakala wake – Felix Majani, Yanga wamefungiwa kufanya usajili wowote kwa kipindi cha miaka 3 mpaka pale watakapo mlipa Tambwe stahiki zake. Endapo klabu hiyo itashindwa kufanya hivyo, watakatwa pointi kwenye VPL na pia watapigwa faini kubwa zaidi.
Afisa habari wa klabu hiyo, Antonio Nugaz amethibitisha kupokea taarifa hiyo kwa kusema kuwa ” kwanza niwaondoe hofu mashabiki wa Yanga kuhusu ishu ya Tambwe, tumepokea taarifa hiyo kupitia kwa katibu mkuu wa klabu – Hajji Mfikirwa na ataifanyia kazi.
“Kama mchezaji anatakiwa kulipwa basi atalipwa bila matatizo yeyote kupitia kwa wadhamini wetu SportsPesa na Brand GSM.” aliiambia Viwanjani Leo.
Neptune’s Richies ni mchezo Unaokupa pesa chap chap huku ukiwa unaburudika kupitia Kasino ya Mtandaoni ndani ya Meridianbet.
Magdalena
Yanga Wana wakati mgumu Sana wa kutoa pesa nyingi Sana
Caroline
Duhh mmeanza figisu figisu
Rahma
Sasa itakuwaje polen sana yanga
Hopemwaikuka
Mlipen hak yake
Dorophina
Pesa nyingi sana lkn inabidi wamlipe haki yake
Sarah
Pole yao yanga chamuhimu wampe haki yake
Fatuma kasomo
Nomaa
Adelta
Yanga mnafeli wapi ??mlipeni tu hiyo ni Haki yake
Amiri Kayera
Wamlipe pesa zake
Mwanahamisi
Noma
Sania
Yanga ni lazima wamlipe huyo mchezaji la sivyo itakula kwao
Lydia Emmanuel Magoti
Duuh sio poa
Khadija
Duh mbona hatari
Venerose
Hatari
Ernest Kimeru
Kazi ipo
Issa
Sa haiwezekan hela ndog kwa gsm
warda
Tena wafungiwe miaka hata sita