Alisema Nicolas Pepe wa Arsenal “kama hauchezi, hauwezi kuwa na furaha”. Olivier Giroud anapitia hayo ndani ya Chelsea, Frank Lampard anasisitiza kumuhitaji mshambuliaji huyo licha ya kusugua benchi kwa muda mrefu.
Giroud anatazamia kufanya maamuzi mapema mwezi Januari endapo hali yake haitobadilika ndani ya kikosi cha Chelsea kwa siku zilizobaki kabla ya dirisha jipya kufunguliwa rasmi.
Hii ni baada ya Kocha wa Chelsea – Frank Lampard kutompa nafasi Giroud kuonesha uwezo wake na zaidi sana anamtumia kama ‘super sub’ kitu ambacho mshambuliaji huyo akubaliani nacho.
Giroud alifanya vizuri sana mwishoni mwa msimu uliomalizika na kuisaidia Chelsea kumaliza kwenye nafasi ya 4 kwenye msimamo wa EPL. Akiwa na timu ya Taifa ya Ufaransa katika Mashindano ya UEFA Nations League, alianza katika mechi 2 kati ya 3 na kupachika magoli 2 katika mchezo dhidi ya Sweden.
Hali ni tofauti msimu huu ndani ya kikosi cha Frank Lampard ambapo Timo Werner na Tammy Abraham wanapewa nafasi zaidi ya kuongoza safu ya mashambulizi ya Chelsea na Giroud akitumika kama mbadala wa wachezaji hao.
Akizungumza na waandishi wa habari, Lampard amesema “Nina mipango na Oli. Ni mchezaji wa muhimu kwenye kikosi chetu.
“Alikuwa wa muhimu sana mwaka jana. Alicheza michezo mingi na alianza kwenye michezo hiyo. Kila siku atahitaji kucheza zaidi na ni mchezaji wa muhimu sana kwenye timu.
“Ninajua ataendelea kuwa mchezaji wa muhimu kwetu kwahiyo ninataka Oli abaki hapa. Ninamahusiano mazuri na Oli na kama alijisikia kwa namna yeyote kwamba hili litabadilika basi nitafurahi kama nitafanya haya mazungumzo na yeye.
“Lakini ninamtaka abaki hapa. Nipo tayari kwa lolote litakalotokea kama kutakuwa na mabadiliko yeyote lakini kwa sasa ni mchezaji wa muhimu kwetu.”
Hadi 130,000,000 TSH Kutolewa kwa washiriki wa shindano la Playson Cashfall. Unaipata kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet Pekee. Jisajili sasa, kisha ingia mchezoni kabla ya Novemba 29.
magdalena
giround yuko vizuri sana
Janeflora malisa
Safi
Sania
Good
Tatu
Kijana yupo vizuri
Lydia Emmanuel Magoti
Yupo vizuri kijana anajua
Ester jackson
Inavyoonekana kocha Frank Lampard anamuhitaji sana mchezaji Giroud labda anaumuhimu nae badae sema tu mchezaji hajamuelewa kutokana na kuwekwa benchi kwa muda ampe tu nafasi nafikiri kocha anaumuhimu mkubwa kwake
Sauda
Jamaa anajituma sana
Angelina
Nice update
Saupha mohamed
Jamaa yupo vizur
Caroline
Giroud mbona yupo vizuri.atapata tu sehemu sahihi
Hopemwaikuka
Ndo umchuke haraka sasa
Fatuma kasomo
Jamaa yupo vizur
Povel
Giroud inabid ajaribu kuangaliah utaratibu wa kuhama chelsea na kutafuta timu yakucheza mara kwa mara ilihawez kukuza kiwango chake na kurudi kwny ubora wake Kama giroud tuliyomzoeha wa kipind hcho
Adelta
Vizuri
aisha
Mchukueni haraka sana wala msilembe
Latifa juma mohamed
Thanteni kwa makala nzur
Latifa juma mohamed
Thanks for gud information.
samiah
Vzr
Rehema
Good
Fatina mfingi
Kijan yuko vizur kwaiy mkilemb shaur yenu!
Rahma
Saf
Mwajumah
Yupo vizuri sana anajua jamaa
Sarah
Good
warda
Lampard anaona mbali sana