Gerard Pique Ana Matumaini na Fainali za Davis Cup

Siku ya Jumapili staa wa kabumbu kutokea klabu ya soka ya Barcelona ya nchini Hispania, Gerard Pique alisema kuwa yeye bado ana matumaini juu ya fainali za michuano ambayo inadhaminiwa na kampuni yake, Davis Cup na kuwa itaendelea katika jiji la Madrid mwaka huu huu.

Kundi la wawekezaji la Pique, Kosmos lina dili la miaka 25 yenye thamani ya jumla ya dola bilioni 3 baina yake na International Tennis Federation!

Hata hivyo, anaamini kuwa mwezi Novemba kati ya tarehe 23-29 kutakuwa na fainali za kombe hilo nchini Hispania katika mji mkuu wa taifa hilo ingawa kuna balaa la ugonjwa wa Corona kwa sasa.

“Mambo hayatabiriki kabisa, tunajaribu kuwa na uelewa wa kitu ambacho serikali itaamua juu ya michezo yote na endapo tutaweza kuwa na mashabiki ama lah ndani ya Caja Magica,” alisema hayo Pique wakati akiongea na kituo cha televisheni cha Movistar.

“Ninaweza kusema kwamba bado nina matumaini makubwa kwa sababu michuano ya Davis Cup bila ya uwepo wa mashabiki haipendezi kabisa.

“Ninafikiri kuwa hakuna mtu ambaye ana uhakika juu ya yatakayokuja kutokea siku za mbeleni na juu ya kuingia uwanjani tukiwa na mashabiki ama bila ya wao kuwepo. Kadri ambavyo siku zinakwenda mbele ndivyo tunaona ni kwa namna gani tutatambua hali itakavyokuwa kiuhalisia zaidi.”

Hispania, moja ya taifa ambalo limeathiriwa sana na ugonjwa huu, limekuwa na majadiliano juu ya namna ya kulegeza baadhi ya masharti ya kukaa ndani wakati huu wa mlipuko wa ugonjwa ambao ulianza kushika hatamu tangu katikati ya mwezi wa tatu mwaka huu.

Kuna mipango kuwa wanaotakiwa kuhudhuria endapo kutakuwa na jukwaa la wazi ni watu wapatao 400 pekee na watu 50 endapo watakuwa ndani ya uwanja.

Hispania ilishinda tuzo ya Davis Cup mwaka 2019, walipowapiga Canada 2-0 katika fainali iliyofanyika kule kule mjini Madrid ikiwa ni toleo la kwanza la michuano hiyo iliyoboreshwa zaidi.

Tangu mwezi wa tatu tarehe za katikati kumekuwa na zuio la uendeshaji wa michuano ya tenisi duniani ambapo pia Wimbledon ilifutwa kwa mara ya kwanza kabisa tangu vita vya pili vya dunia viishe na Roland Garros ikahamia mwezi Septemba na Oktoba mwaka huu.

Inatarajiwa kuwa ATP na WTA itarejea tena ifikapo JUlai 13 mwaka huu endapo mambo yakiwa sawa kiafya.

20 Komentara

    sante kwa taarifa vzr. mmoja wa mabeki bora wazuri.#meridianbettz

    Jibu

    Mungu aepushe tu hili janga la corona na pique matumaini yake yatakuwa sahihi

    Jibu

    Nashukulu kwa taarifa

    Jibu

    daah!!! kumbe pique sio mpila tuu, hata tennis yupo, safi sana

    Jibu

    meridianbet hamjawai kuboa

    Jibu

    Asante meridian kwa habar Moto Moto za Kimichezo meridian bet tz#

    Jibu

    Good news 👍@ meridianBetTZ

    Jibu

    gerard yuko vzr namkubali uyu beki

    Jibu

    Well said Gerard Pique.

    Jibu

    asanteni kwa taarifa nzuri meridian

    Jibu

    Itakua imekaa poa kwa Gerard

    Jibu

    ahsante kea taarifa meridian nawakubali sana

    Jibu

    Ni taarifa nzuri tunashukuru meridianbet kutujulisha.

    Jibu

    Meridiani mpo vizuri hamchelewi kutupa taarifa watu wenu asanteni👏

    Jibu

    Aisee ni michezo yote bila mashabiki hainogi kabisaa

    Jibu

    Nice #meridianbettz

    Jibu

    meridianbet mko juu #meridianbettz

    Jibu

    Asante meridianbet kwa taarifa

    Jibu

    Itakuwa poa.

    Jibu

    Gerrad pique alikuwa beki bora San nadani ya klabu ya Barcelona pia habari nzuri meridianbettz Asante kwa taarifa

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.