Serge Gnabry anajiandaa kukaa nje ya dimba baada ya kupata jeraha la misuli katika paja lake la mguu wa kushoto Bayern Munich yathibitisha.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ujerumani alitolewa nje dakika ya 64 ya mchezo katika fainali ya Club World Cup ambapo Bayern Munich iliibuka na ushindi wa 1-0 na kuwa mabingwa wapya wa mashindano hayo.
Mabingwa wa Bundesliga Bayern Munich hawajaweka wazi ni kwa muda gani mchezaji huyo wa miaka 25 atakaa nje ya dimba ambapo pia walikuwa bila Thomas Muller ambaye alikutwa na maambukizi ya Coronavirus jijini Qatar.
Taarifa rasmi ya klabu ilisomeka: “Kwa muda uliyopo Bayern watakuwa bila Serge Gnabry.
“Mshambuliaji amepata jeraha la misuli katika paja lake la mguu wakushoto siku ya jana katika fainali ya Club World Cup dhidi ya Tigres. Haya yalikuwa na majibu ya vipimo viliyofanywa na idara ya matibabu ya Bayern Munich.
Baada ya kushinda Club World Cup, Bayern watarudi dimbani kuchuana na Arminia Bielefeld siku ya Jumatatu wakiwa nyumbani mchezo wa Bundesliga.
Kisha watacheza dhidi ya Lazio katika michuano ya Champions League hatua ya 16 bora Februari 23 harafu watawakabili Borussia Dortmund mwezi March.
Unaweza kuvuna mkwanja mrefu kadiri uwezavyo kupitia mchezo wa Gold n Rocks kwenye kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Ni rahisi! Vigezo na masharti, kuzingatiwa.
Magdalena
Pole Sana ndo changamoto za kazi
Adelta
Pole yake
Sadick
Bayern inamuhitaji sana Gnabry kwasasa kuliko wakati mwingine wowote kutokana na kukabiliwa na majeruhi ktk nafasi muhimu
Dorophina
Pole gnabry
Caroline
Pole sana
Sania
Majeraha sio poa kabisa
Mwanahamisi
Pole yake
Samira
Bayarn imekabiliwa sana na mejeruhi tena wote wamuhimu
Lydia Emmanuel Magoti
Pole yake
Hopemwaikuka
Pole kwako
warda
pole yake