Kocha wa Simba, Didier Gomes amesisitiza kwamba sasa akili zao wameelekeza DR Congo kwenye mechi dhidi ya AS Vita hii na lazima wafanye kitu.
βTunatambua tunaenda kukutana na timu kubwa ambayo shauku yake ni kushinda mechi ya kwanza ya hatua ya makundi kama ilivyo kwetu, tunajiamini na wachezaji wangu wote wapo kwenye ari nzuri ya ushindani na tupo tayari kwa mapambano.
βMashindano ya Simba Super Cup yalitupa mwanga wa wapi pa kuanzia, ukiangalia kwenye michezo yetu minne iliyopita dhidi ya Al Hilal, TP Mazembe, Dodoma Jiji na Azam tumeongoza kwa kutengeneza nafasi za mabao kuliko timu yeyote ile hivyo hicho ni kiashiria kuwa tunaweza kupata matokeo chanya mbele ya timu yeyote ile,β
alisema Gomes ambaye ana uzoefu na mechi za Afrika akiingoza El Merreikh ya Sudan kuwazuia Enyimba ya Nigeria kutinga makundi ya Afrika nyumbani kwao.
βNi kweli mechi dhidi ya Azam wachezaji wamekosa mabao mengi ya wazi lakini hicho sio kigezo cha kuwabeza, kuwaadhibu ama kusema sio bora kwani hayo mambo yanatokea kwenye soka kikubwa ni kuendelea kuyafanyia kazi makosa yale ili yasiwe yanajirudia mara kwa mara,β aliongeza Gomes.
Unaweza kuvuna mkwanja mrefu kadiri uwezavyo kupitia mchezo wa Gold n Rocks kwenyeΒ kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Ni rahisi! Vigezo na masharti, kuzingatiwa.
Angelina
Naamini simba watafanya vizuri
Sania
Simba hawashindwi
Magdalena
Simba wamejipanga Sana na wapo tayari kuwakabiri kivyovyote
Sadick
Utakuwa mchezo mgumu hasa ikizingatiwa walishaifunga Simba bao 5 mwaka 2019.
Dorophina
Simba watawaweza kweli AS vita au maneno tu
Lydia Emmanuel Magoti
Mchezo huo atutauwachia Wana Simba lazima tukaze
Rahma
Ngoja tuone
Issa
Vita 5 simba 0
Sarah
Tunasubiri tuone
Hopemwaikuka
Kaz kaz
warda
Simba round hii wanajiamini sana