Meneja wa Man City Pep Guardiola yupo kwenye sintofahamu juu ya Sergio Aguero, na anakiri kuwa haoni kama kuna haja ya kumharakisha staa huyu kurejea dimbani.
Guardiola anaamini kuwa staa huyu atarejea kwenye fomu yake kama kawaida, japokuwa hilo linahitaji muda na mechi pia za kutosha.
Meneja huyu anasema kuwa katika mipango yake ya kuchagua kikosi kwa sasa anahitaji sana kuchagua kikosi kwa kuzingatia wachezaji ambao wapo kwenye fomu zaidi wakiwa wanapambana kukamata taji jingine msimu huu.
Aguero alipata kuanza kwenye mechi kwa mara ya kwanza baada ya miezi minne wakati vinara wa Ligi ya Uingereza wakipata ushindi wao wa 20 mfululizo wa 2-1 djidi ya West Ham pale Etihad Stadium Jumamosi.
Nyota huyu alikosa sehemu kubwa ya mwanzo wa msimu kutokana na jeraha la goti alilokuwa nalo, na baada ya kufanyiwa upasuaji suala la kurejea dimbani lilikuwa gumu zaidi.
Ni Muda wa Kuvuna Mkwanja na Jungle Jim and the Lost Sphinx
Hauihitaji kufikira mara mbili ni mchezo gani utakupatia mkwanja ndani ya kasino za Meridianbet. Jiunge sasa ufurahie Jungle Jim and the Lost Sphinx.
Man City mko vinzur
Guardiola anajidai sana
Nice update
Yuko sahihi
Yuko sawa
Anaona yupo juu
Nc