Thiago Alcantara hatarejeshwa mapema kuanza dimbani licha ya kurejea kufanya mazoezi na kikosi cha kwanza, kwa mujibu wa bosi wa Liverpool Jurgen Klopp.
Nyota huyu raia wa Hispania ameshindwa kuwepo dimbani kwa zaidi ya miezi miwili sasa tangia alipopatikana na jeraha la goti kwenye debi ya Merseyside dhidi ya Everton mwezi Oktoba.
Nyota huyu pia alipatikana na maambukizi ya Corona, kitu kilichomfanya akose mechi nyingi zaidi. Amecheza mara mbili tu akiwa na klabu ya Liverpool tangia alipowasili klabuni hapo kutokea Bayern Munich.
Staa huyu wa miaka 29 amerejea kufanya mazoezi na kikosi kizima cha timu ya Liverpool mapema Jumatano. Hata hivyo, kwa mujibu wa Klopp, kumchezesha kwenye mechi ijayo, ya Jumapili dhidi ya West Brom bado itakuwa ni mapema sana kwa nyota huyu kurejea dimbani.
Klopp anaamini Xherdan Shaqiri na James Milner wanaweza wakarejea na kuwa msaada wakati, Thiago Alcantara akiendelea kusubiri.
“Thiago tayari ameshapiga hatua moja katika mazoezi ya timu. Bado hajaanza kujumuishwa moja kwa moja kwenye mazoezi kwa ujumla lakini ameanza kupiga hatua nzuri, kwa bahati mbaya baada ya mda mrefu, hatuwezi na hatutamuwahisha.”
– Klopp akizungumzia hatua ya kutejea kwa Thiago Alcantara
VUNA SHEA YAKO YA 230,000,000TSH NA UFURAHIE MSIMU HUU WA SIKUKUU!!!
Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, jiwekee nafasi ya kupata shea yako ya 230,000,000Tsh kupitia mchezo wa Secret Santa. Hakika hutojutia kufurahia msimu huu wa sikukuu ukiwa katika nyumba ya mabingwa ya Meridiabet. Unasubiri nini???
Issa
Liver kafika
Hopemwaikuka
Ni vzur pia
Adelta
Bado mashabiki tunamkubali
Tatu
Ni vizuri
Sarah
Tunamkubali sana mashabiki
Shakila mrope
Safi sana
Caroline
Pole Sana
Angelina
Goodnews
Rahmal
Ni vizuli
Saupha mohamed
Nice
Ernest Kimeru
Ni vizuri ili kusaidia Thiago Alcantara aweze kurudi kwenye fomu yake
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri
warda
Kama amepona acheze tu